TTB YAADHIMISHA MIAKA 61 YA UHURU WA TANZANIA KWA KUSHIRIKI KATIKA MAONESHO YA SANAA

Picha ya Pamoja, Dkt. Soumya Manhunath Chavan na watumishi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).
Mkuu wa Kituo cha Kutolea Taarifa kwa Watalii cha Bodi ya Utalii kanda ya Pwani, Alistidia Karaze akimkabidhi Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni wa India, Dkt. Soumya Manhunath Chavan mfuko wenye zana za kutangazia utalii mara baadaya kufungia maonesho ya sanaa.


Mmoja ya wasanii walioshiriki Maonesho ya Sanaa.

************************

Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imeshiriki katika maonesho ya Sanaa ya Uchoraji wa Picha mbalimbali zinazoonyesha mandhari ya vivutio vya utalii vya Tanzania, Maonesho haya yana lengo la kukuza kazi ya Sanaa ili wasanii waweze kujikwamua kiuchumi na jamii iweze kuitambua na kuithamini kazi ya sanaa ya uchoraji.



Maonesho haya ya siku tatu yameandaliwa na Jumuiya ya Kihindi inayoitwa Arthshakti Foundation kama sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania, Maonesho ya Sanaa yanafanyika katika Mgahawa wa Chill a& Lime uliopo jijini Dar es salaam, Kuanzia leo Disemba 9 – 11, 2022.



Akiongea mara baadaya ufunguzi wa Maonesho Mkuu wa Kituo cha Kutolea Taarifa kwa Watalii cha Bodi ya Utalii kanda ya Pwani, Alistidia Karaze amesema”

Tunawashuri vijana wanaochipukia katika sanaa ya uchoraji, kuendelea nayo pasipo kukta tamaa kwani Sanaa ya uchoraji ni njia mojawapo ya kutangaza utalii kupitia picha vile vile na kukuza uchumi na kuongeza ajira”.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments