TBS YATOA ELIMU NAMNA YA KUPATA ALAMA YA UBORA KWA WAJASIRIAMALI SINGIDA

Meneja Uhusiano na Masoko ( TBS), Bi. Gladness Kaseka akitoa maelezo kuhusu utaratibu wa kupata leseni ya kutumia alama ya ubora ya TBS bila gharama yoyote kwa baadhi ya Wajasiriamali wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

TBS ilitoa elimu hiyo wakati wa kampeni ya elimu kwa Umma kuhusu viwango mkoani Singida.


Mkaguzi (TBS) , Bw. Magesa Mwizarubi akitoa elimu kuhusu utaratibu wa kusajili majengo ya chakula na vipodozi pamoja na umuhimu wa kusoma taarifa zilizopo katika bidhaa hususani muda wa mwisho wa matumizi kwa wafanyabiashara katika Stendi mpya, Stendi ya zamani na Soko Kuu mkoani Singida. TBS iliwakumbusha wafanyabiashara wa chakula na vipodozi mkoani Singida kufanya usajili wa majengo ili kuepuka usumbufu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments