RAFIKI - SDO WAKUTANISHA BARAZA LA WATOTO NGAZI YA HALMASHAURI KUWASILISHA CHANGAMOTO ZA WATOTO KWA WATOA MAAMUZI



Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga John Tesha, akizungumza kwenye kikao hicho cha Baraza la watoto ngazi ya Halmashauri.


Meneja wa Mradi wa Uimarishaji wa Mabaraza ya watoto (MKUA) kutoka Shirika la Rafiki-SDO Tangi Clement, akizungumza kwenye kikao cha Baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi Manispaa ya Shinyanga.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

SHIRIKA la Rafiki-SDO ambalo linajihusisha na utetezi wa haki za watoto, limekutanisha baraza la watoto ngazi ya Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, pamoja na watoa maamuzi wa Halmashauri hiyo, ili kuwasilisha changamoto zinazowakabili watoto na kufanyiwa kazi.
 
Kikao hicho kimefanyika leo Desemba 12, 2022 katika ukumbi wa Shypark Hotel, kwa kukutanisha watoto ambao ni Wenyeviti wa Mabaraza ya watoto ngazi ya Kata zote 17 za Manispaa ya Shinyanga, wakiwamo na walimu wao walezi wa Mabaraza hayo, pamoja na watoa maamuzi ambao ni Wakuu wa idara Manispaa ya Shinyanga.

Meneja wa Mradi wa Uimarishaji wa Mabaraza ya watoto (MKUA) kutoka Shirika la Rafiki-SDO Tangi Clement, amesema Shirika hilo limefanikiwa kuunda Mabaraza ya watoto katika Mitaa 28 na vijiji 17 vya manispaa ya Shinyanga, pamoja na madawati 77 ya watoto shule, ambapo shule za Msingi madwati 57 na Sekondari 20, lengo ni kuwaweza watoto waweze kupaza sauti kwenye masuala yote yanayohusu watoto vikiwamo vitendo vya ukatili.

Amesema baada ya kumaliza kuunda Mabaraza hayo ya watoto ngazi ya Mitaa na Vijiji, wakawajengea uwezo ili watoto watambue wajibu wao na haki zao, ndipo watoto hao wakaomba wakutane na watoa maamuzi wa Manispaa ya Shinyanga ili kuwaeleza changamoto ambazo watoto wanakumbana nazo na kutafutiwa ufumbuzi.

“Mabaraza haya ya watoto yana msaada mkubwa katika kupambana na vitendo vya ukatili kwa watoto, sababu watoto ni virahisi kuambiana wenyewe juu ya vitendo vya ukatili ambavyo wanafanyiwa,”amesema Tangi.

Nao viongozi hao wa Mabaraza ya watoto ngazi ya Kata, waliwasilisha changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili watoto katika maeneo yao, zikiwamo za ukosefu wa miundombinu rafiki shuleni, upungufu wa madawati katika shule za msingi na vifaa vya kujifunzia.

Changamoto zingine upungufu wa walimu wa masomo ya Sayansi shule za Sekondari, hakuna Maabara, vyumba maalum vya kujistili hedhi, huku wakiomba pia suala la ulaji chakula shuleni lizigatiwe kwa shule zote, kudhibiti majanga ya moto shuleni, pamoja na kushirikishwa kwenye uaandaji wa bajeti za Halmashauri na kuingizwa kwenye Kamati za Mtakuwwa na kupatiwa usafiri wa mabasi madogo kwenda shule.

Pia watoto waliomba Manispaa itenge Bajeti kwa ajili ya maadhimisho mbalimbali ya siku ya watoto.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga John Tesha, akizungumza kwenye mkutano huo, amelipongeza Shirika la Rafiki-SDO pamoja na wadau wengine kwa kuunda Mabaraza ya watoto na kuifanya Manispaa hiyo kuwa ya kwanza kukamilisha zoezi la uishwaji wa mabaraza ya watoto kutoka na muongozo mpya wa kitaifa.

Aidha, amewataka watoto wayatumie vyema Mabaraza hayo kupasa sauti juu ya vitendo vya ukatili ambavyo wanafanyiwa ili hatua za haraka zipate kuchukuliwa kabla ya kuleta madhara.

Amesema changamoto zote ambazo wameziwasilisha watoto hao, nyingine tayari zipo kwenye utekelezaji na nyingine zitafanyiwa kazi,likiwamo suala la usafiri kwa watoto, ambapo mwakani Halmashauri hiyo itatoa Hiace Sita za mikopo kwa vijana, lakini masharti yake ni kupeleka shule kwanza watoto na kuwafuata jioni kwa nauli ya Sh.200 hadi 300.

Pia akijibu maombi ya watoto kushirikishwa kwenye mchakato wa uundaji wa bajeti za Halmashauri, amesema kwa sasa Manispaa ipo kwenye uandaaji wa bajeti hivyo kwenye vikao vya kamati vya bajeti watashirikishwa watoto kupitia viongozi wao Mwenyekiti na Katibu.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga John Tesha, akizungumza kwenye kikao hicho cha Baraza la watoto ngazi ya Halmashauri.

Afisa utumishi Manispaa ya Shinyanga Getruda Gisema akizungumza kwenye kikao hicho cha Baraza la watoto.

Afisa Maendeleo ya Jamii Sifa Amon akizungumza kwenye kikao hicho.

Meneja wa Mradi wa Uimarishaji wa Mabaraza ya watoto (MKUA) kutoka Shirika la Rafiki-SDO Tangi Clement, akizungumza kwenye kikao hicho cha Baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi Manispaa ya Shinyanga.

Meneja wa Mradi wa Uimarishaji wa Mabaraza ya watoto (MKUA) kutoka Shirika la Rafiki-SDO Tangi Clement, akizungumza kwenye kikao hicho cha Baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi Manispaa ya Shinyanga.

Mdau wa watoto John Eddy akizungumza kwenye kikao hicho.

Wakuu wa Idara Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye kikao cha Baraza la watoto ngazi ya Halmashauri wakisikiliza uwasilishwaji wa kero za watoto na kuona namna ya kuzitafutia ufumbuzi.

Viongozi wa Mabaraza ya watoto wakiwasilisha kero za watoto kwenye kikao hicho.

Viongozi wa Mabaraza ya watoto wakiwasilisha kero za watoto kwenye kikao hicho.

Viongozi wa Mabaraza ya watoto wakiwasilisha kero za watoto kwenye kikao hicho.

Viongozi wa Mabaraza ya watoto wakiwasilisha kero za watoto kwenye kikao hicho.

Kikao cha viongozi wa baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi kikiendelea.

Kikao cha viongozi wa baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi kikiendelea.

Kikao cha viongozi wa baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi kikiendelea.

Kikao cha viongozi wa baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi kikiendelea.

Kikao cha viongozi wa baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi kikiendelea.

Kikao cha viongozi wa baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi kikiendelea.
Kikao cha viongozi wa baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi kikiendelea.

Kikao cha viongozi wa baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi kikiendelea.

Kikao cha viongozi wa baraza la watoto ngazi ya Halmashauri na watoa maamuzi kikiendelea.

Walimu ambao ni walezi wa Mabaraza ya watoto wakiwa kwenye kikao hicho.

Walimu ambao ni walezi wa Mabaraza ya watoto wakiwa kwenye kikao hicho.

Walimu ambao ni walezi wa Mabaraza ya watoto wakiwa kwenye kikao hicho.

Walimu ambao ni walezi wa Mabaraza ya watoto wakiwa kwenye kikao hicho.

Picha ya Pamoja ikipigwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments