KAMATI YA MAWAZIRI 8 WA KISEKTA YAWASILI MKOANI KAGERA


Kamati ya Mawaziri Nane wa Kisekta imewasili rasmi mkoani Kagera kwa ajili ya kuongea na wakazi wa vijiji vinne vya kata ya Rutoro kuhusu uamuzi wa Baraza la Mawaziri juu ya vijiji hivyo ambavyo vimo ndani ya eneo la Ranchi ya Kagoma wilayani Muleba mkoa wa Kagera.

Kamati hiyo inaongozwa na mwenyekiti wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba ndaki na Makamu wake Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Ridhiwani Kikwete.

Wengine ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mary Masanja, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. David Silinde, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Anthony Mavunde, Naibu Waziri wa Maji Mhe. Eng. Maryprisca Mahundi, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Khamis Chilo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments