Picha : SAMIA DAY YATIKISA SHINYANGA!! KATAMBI ATINGISHA... 'ASANTE MAMA TUMEKUELEWA KAZI IENDELEE'


Makada wa CCM wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu wakicheza muziki wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Kada wa CCM, Toffee Uptown akiwa ameshikilia picha ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Maadhimisho ya Siku Maalumu ya Kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan iliyopewa jina la ‘SAMIA DAY’ ikiongozwa na Kauli Mbiu ‘Asante Mama Tumekuelewa na Kazi Iendelee’ iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi yamefanyika mkoani Shinyanga.


Samia Day iliyolenga kumshukuru na kumpongeza Rais Samia kwa mambo mbalimbali aliyoyafanya ndani ya Mkoa wa Shinyanga kwa kipindi cha miaka miwili tangu awe Rais wa Tanzania imefanyika leo Alhamisi Desemba 15,2022 katika Uwanja wa Zimamoto Mjini Shinyanga ambapo Mgeni rasmi alikuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mabala Mlolwa.


Akizungumza katika Maadhimisho hayo,Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu amesema Mkoa wa Shinyanga una kila sababu ya kumpongeza Rais Samia kwa mambo mbalimbali ya maendeleo aliyofanya katika sekta zote ikiwemo elimu, afya,maji na miundombinu.


“Asante Mama Samia Suluhu Hassan, Shinyanga Tumekuelewa na Kazi Iendelee”, amesema Katambi.


“Hiki siyo kipindi cha kufanya majungu, mmetutuma kufanya kazi siyo kuleta umbea, mimi hasira yangu ni kuleta maendeleo…Wakati wa kupigana vijembe umeisha, kazi iliyobaki ni kuleta maendeleo. Ni wakati wa ujenzi wa Shinyanga yetu,tutaendelea kuleta miradi mbalimbali ya maendeleo lengo ni kuhakikisha kunakuwa na mzunguko wa fedha mkoani Shinyanga”,ameongeza Katambi.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mabala Mlolwa amesema Rais Samia amefanya mambo makubwa ndani ya miaka miwili ambayo hayajawahi kufanyika tangu nchi ipate Uhuru.


MheRais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kipindi cha miaka miwili ya uongozi wake amefanya mambo ambayo alipaswa kuyafanya kwa kipindi cha miaka mitano, Shinyanga tunamshukuru na tunampongeza sana”,amesema Mabala.
Makada wa CCM wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu wakicheza muziki wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Makada wa CCM wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu wakicheza muziki wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Makada wa CCM wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu wakicheza muziki wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Makada wa CCM wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu wakicheza muziki wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza Mbunge wa Jimbo la Shinyanga akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Kada wa CCM, Toffee Uptown akiwa ameshikilia picha ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Kada wa CCM akiwa ameshikilia bango wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.


Kada wa CCM akiwa ameshikilia bango wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Mhe. Anord Makombe akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mabala Mlolwa akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mabala Mlolwa akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko akizungumza wakati wa Samia Day leo Mjini Shinyanga.
Wakazi wa Shinyanga wakiwa kwenye maadhumisho ya Samia Day.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments