MWANAFUNZI AFARIKI AKIDAIWA KUPIGWA NA MWALIMU ALIVYOSHINDWA KUJIBU SWALI DARASANI




Mama wa marehemu Amina

***

Mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya sekondari Sabasaba, Manispaa ya Mikindani mkoani Mtwara, Amina Ally, (16), anadaiwa kufariki dunia baada ya kupigwa na mwalimu wake kwa kushindwa kujibu swali darasani, na kupelekea kudondoka na kupoteza fahamu akiwa shuleni hapo.


Marehemu anadaiwa kufanyiwa kitendo hicho Oktoba 20 mwaka huu, na mwalimu aliyafahamika kwa jina la Masumbuko, na kwamba amefariki dunia jana Desemba 20, 2022, wakati alipokuwa akiendelea kupatiwa matibabu.

Juma Hassan ni ndugu wa marehemu ambapo pamoja na mambo mengine akaeleza uchugunzi uliofanywa na madaktari ambapo umebaini kwamba mishipa ya pua ilikuwa imekatika hali iliyopelekea kuvuja damu muda wote, huku akitoa ombi kwa serikali.

CHANZO - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments