SELEMAN MPEPE WA NANYUMBU ABONGEKA NA BIKOSPORTS

Mkazi wa Nanyumbu mkoani Mtwara, Selemani Mpepe, aliyenyoosha mikono juu, akiwa na marafiki zake baada ya kufanikiwa kukabidhiwa fedha zake Sh Milioni 4 alizoshinda kama sehemu ya bonasi Bonge kutoka kwenye mchezo wa kubashiri matokeo ya michezo mbalimbali duniani wa Bikosports.
Mkazi wa Nanyumbu mkoani Mtwara, Selemani Mpepe, akiwa na furaha kubwa baada ya kufanikiwa kukabidhiwa fedha zake Sh Milioni 4 alizoshinda kama sehemu ya bonasi Bonge kutoka kwenye mchezo wa kubashiri matokeo ya michezo mbalimbali duniani wa Bikosports.

MKAZI wa Nanyumbu mkoani Mtwara, Selemani Mpepe, ameibuka na bonasi bonge ya kiasi cha Sh Milioni 4 kutoka kwenye mchezo wa kubashiri matokeo wa bikosports unaoendelea kumwaga manoti kwa Watanzania wanaotumia bikosports kuweka mikeka yao.

Akizungumza katika makabidhiano ya zawadi hiyo ya fedha, Mpepe amesema zawadi hiyo aliyoipata kama bonasi imefungulia njia nzuri katika maisha yake sanjari na kupunguza makali.

Amesema amekuwa akitumia mchezo wa Bikosports kama njia ya kutafuta njia ya kutimiza malengo yake, akiamini kuwa ni sehemu nzuri inayoweza kumpatia ufumbuzi wa maisha yake.

“Katika mkeka wangu niliweka mechi nane na kuingiza kiasi cha 40,000 kama mtaji wangu, jambo ambalo lilinipatia kiasi cha fedha ambacho kitasogeza mbele gurudumu la maisha yangu.

“Nitatumia kiasi cha pesa katika biashara zangu ndogo ndogo ambazo siku zote nimekuwa nikizifanya kwa lengo la kunipatia mwangaza mzuri zaidi,” amesema.

Mchezo wa kubashiri matokeo ya michezo mbalimbali duniani ni rahisi kucheza na kushinda ambapo namba ya Kampuni ni 101010, huku ukitoa fursa ya kucheza live mtandaoni kwa www.bikosports.co.tz bila kusahau wanaobeti njia ya kwa kupiga *149*89# wakitumia pia 101010 kama namba ya kampuni ya Bikosports.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments