SIMBA SC YALAZIMISHWA SARE 1-1 MBEYA CITY


*********************

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Simba imelazimishwa sare ya mabao 1-1 dhidi ya timu ya Mbeya City, mchezo ambao ulipigwa kwenye dimba la Sokoine Mbeya.

Katika mchezo huo Simba Sc ilianza kupata bao katika kipindi cha kwanza kupitia kwa kiungo wao Mzamiru Yasin dakika ya 15 na kuwapelaka mapumziko wakiwa wanaongoza kwa bao 1-0.

Kipindi cha pili klabu ya Mbeya City iliingia ikiwa inahitaji kusawazsiha bao kwani walicheza mpira wa kushambulia bila mafanikio mpaka dakika za lala salama kupata bao la kusawazisha kupitia kwa Tariq Seif dakika ya 78.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments