WAZIRI WA MADINI DOTTO BITEKO ATEMBELEA WAATHIRIKA WA TOPE BWAWA LA MGODI WA ALMASI MWADUI


Waziri wa Madini Dotto Biteko wapili (katikati) akiangalia eneo ambalo limeathiriwa na Tope la Bwawa la Mgodi wa Almasi Mwadui mara baada ya kupasuka kingo zake.

Na Marco Maduhu. KISHAPU

WAZIRI wa Madini Dotto Biteko ametembelea wananchi ambao wameathirika na Tope la Mgodi wa Almasi Mwadui mara baada ya bwawa lake kupasuka na kutiririsha tope kwenye makazi yao na kutaka wananchi waelezwe ukweli kama tope hilo linasumu ama laa.

Biteko amefanya ziara hiyo leo Novemba 10, 2022 kwa kutembelea waathirika hao pamoja na kuona eneo ambalo limeathiriwa na tope la mgodi huo wa Mwadui.

Akizungumza na uongozi wa Mgodi huo, amewataka wafanya tathimini ya haraka ya kubaini athari ambao wamezipata wananchi na kuwalipa fidia, pamoja na kudhibiti tope hilo lisiendelee zaidi kwenda kwenye makazi ya wananchi hasa katika kipindi hiki cha mvua.

“Nawapongeza uongozi wa Mkoa wa Shinyanga pamoja na Mgodi mara baada ya bwawa hili kupasuka kitu cha kwanza kabisa mlijali usalama wa wananchi na hakuna ambaye amepoteza maisha zaidi ya kupoteza mashamba yao pamoja na nyumba zao na visima vya maji kuzingirwa na tope,”amesema Biteko.

“Kwa sasa Serikali haiwezi kutoa majibu juu ya hatua ambazo itazichukua sababu bado kuna uchunguzi unafanyika na majibu yakitoka ndipo tuta tamka adhabu ambayo mgodi huu unapaswa kuwajibishwa na liwe fundisho kwa wengine kwa kuonyesha uzembe wa hali ya juu, kwa sasa tuna angalia usalama wa wananchi kwanza, na pia waelezwe ukweli kama tope hilo lina sumu au hapana”ameongeza

Aidha, amesema kwa taarifa za awali alizokuwa nazo bwawa hilo la Mgodi wa Almasi Mwadui lilipata hitilafu tangu mwezi wa Tisa mwaka huu, lakini Mgodi huo uliendelea kulitumia na hatimaye limeleta athari kwa wananchi.

Mhandisi Mkuu wa Mgodi huo Mwadui Shagembe Mipawa, amekiri bwawa hilo la mgodi kuwa na hitilafu mwezi huo wa tisa, na walilitolea taarifa kwa uongozi wakaziba sehemu ambazo zilikuwa zina vuja na wakajiridhisha kuwa lipo salama, lakini wanashaghaa siku hiyo novemba 7 likapasuka na tope kuvamia makazi ya wananchi.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Mgodi wa Mwadui Ayubu Mwenda, amesema kitu cha kwanza walichokifanya baada ya kupasuka kwa bwawa hilo ni kuwahi usalama wa wananchi kwanza, pamoja na kuweka matuta ya kuzuia tope hilo lisiendelee kwenda kwenye makazi ya watu zaidi.

Amesema kwa watu ambao wameathirika na tope hilo wapatao 115 wamewahamishiwa kwenye hosteli za mgodi huo na wanaendelea kuwapatia maradhi yote, pamoja na watoto wao kuwapeleka shule na kuwarudisha ili wasiathirike kimasomo huku wakiwatimizia mahitaji yote.

Amesema mgodi huo bado unaendelea kufanya tathimini ili kujua ni kiasi gani wananchi wameathirika ikiwamo kupoteza nyumba pamoja na mashamba, na kuangalia namna ya kuwapatia fidia, huku wakiendelea kuwapatia huduma ya chakula, maji, na matibabu

Akizungumzia tope hilo kuwa na sumu, amesema Kemikali ambazo wanazitumia kwenye mgodi huo hazina madhara kwa binadamu, sababu uzalishaji wa Almasi ni tofauti na dhahabu na kuwatoa wasiwasi wananchi juu ya afya zao.

Naye Meneja wa Mamlaka ya udhibiti na uhifadhi wa mazingira (NEMC) Kanda ya Ziwa Kayombo Jarome, amesema kuna uharibifu mkubwa wa mazingira ambao umetokea, lakini bado wanasubili majibu kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kujua kama tope hilo kama lina kemikali ambazo zina madhara kwa wananchi ndipo watatoa taarifa kamili.

Mbunge wa Jimbo la Kishapu Boniphace Butondo, ameiomba ifanyike tathimini ya haraka ili wananchi wapatiwe maeneo mengine ya mashamba na kufanya shughuli za kilimo, ili kukabiliana na baa la njaa hapo baadae, pamoja na kutekelezewa miradi ya maji safi na salama kutoka Ziwa Victoria.

Nao baadhi ya wananchi akiwamo Meya Ndole, amesema nyumba yake imezingirwa na maji na amepoteza mbuzi wawili ambao walisombwa na tope hilo na kuishukuru Serikali kwa kuwatoa kwenye maeneo ambayo ni hatarisha na kuja kuishi ndani ya mgodi kwa muda.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Sophia Mjema, amewatoa wananchi wasiwasi kuwa Serikali ipo pamoja nao na kila mtu atapata haki yake na hakuna ambaye atapoteza na kuwataka wawe na subira wakati taratibu zingine za kisheria zikifuata.

Waziri wa Madini Dotto Biteko akizungumza na waathirika wa Tope la Bwawa la Mgodi Mwadui, ambao kwa sasa wanaishi ndani ya Mgodi huo.

Waziri wa Madini Dotto Biteko akizungumza na waathirika wa Tope la Bwawa la Mgodi Mwadui, ambao kwa sasa wanaishi ndani ya Mgodi huo.

Mbunge wa Jimbo la Kishapu Boniphace Butondo akizungumza na waathirika wa Tope la Bwawa la Mgodi wa Mwadui, ambao kwa sasa wanaishi ndani ya mgodi huo.

Mbunge wa Jimbo la Kishapu Boniphace Butondo akisalimia na waathirika wa Tope la Bwawa la Mgodi wa Almasi Mwadui.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Sophia Mjema, akizungumza na waathirika wa Tope la Bwawa la Mgodi wa Mwadui, ambao kwa sasa wanaishi ndani ya mgodi huo.

Meneja Mkuu wa Mgodi wa Almasi Mwadui Ayubu Mwenda akizungumza kwenye ziara ya Waziri wa Madini Dotto Biteko.

Wananchi ambao ni waathirika wa Tope la Bwawa la Mgodi wa Almasi Mwadui wilayani Kishapu wakiwa kwenye makazi yao ya muda ndani ya mgodi huo.


Wananchi ambao ni waathirika wa Tope la Bwawa la Mgodi wa Almasi Mwadui wilayani Kishapu wakiwa kwenye makazi yao ya muda ndani ya mgodi huo.

Wananchi ambao ni waathirika wa Tope la Bwawa la Mgodi wa Almasi Mwadui wilayani Kishapu wakiwa kwenye makazi yao ya muda ndani ya mgodi huo.

Waziri wa Madini Dotto Biteko wapili (kushoto) akiangalia eneo ambalo limeathiriwa na Tope la Bwawa la Mgodi wa Almasi Mwadui mara baada ya kupasuka kingo zake.
Waziri wa Madini Dotto Biteko wapili (katikati) akiangalia eneo ambalo limeathiriwa na Tope la Bwawa la Mgodi wa Almasi Mwadui mara baada ya kupasuka kingo zake.

Muonekano wa Kingo ambayo imepasuka kwenye Bwawa la Mgodi wa Alamsi Mwadui la kuhifadhia maji machafu.

Muonekano wa Tope ambalo limesambaa na kwenda kwenye makazi ya watu likitoka kwenye Bwawa la Mgodi wa Almasi Mwadui.

Muonekano wa Tope ambalo limesambaa na kwenda kwenye makazi ya watu likitoka kwenye Bwawa la Mgodi wa Almasi Mwadui.

Ziara ya kuangaliwa eneo ambalo limeathitika na Tope la Bwawa la Mgodi wa Almasi Mwadui ikiendelea.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments