AJALI YA BASI, LORI YAUA NA KUJERUHI DODOMA

 


Watu Sita wamefariki dunia na wengine 22 wakijeruhiwa katika ajali iliyohusisha basi la Arusha Express lenye usajili wa namba T 530 AGG kugongana uso kwa uso na lori Mchanga kampuni ya SINO-HYDRO lenye namba T 939 DZE.

Ajali hiyo imetokea leo Jumapili Novemba 13, 2022 mchana eneo la Veyula Kata ya Makutupora mkoani Dodoma.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amesema waliofariki wote ni wanaume huku Majeruhi 10 wakiwa ni Wanawake na 12 ni Wanaume.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments