MBUNGE ALIYEENDESHA GARI HUKU AMELEWA AJIUZULU


Mbunge wa bunge la Rwanda Gamariel Mbonimana ametangaza kujiuzulu baada ya kukumbwa na tuhuma za kuendesha gari akiwa amelewa.

Mbonimana ametangaza kujiuzulu huku akiomba msamaha kwa Rais Paul Kagame na kuapa kwamba ameamua kuacha kunywa pombe

Katika akaunti yake ya Twitter mbunge huyo alisisitiza zaidi kwamba atajitolea kutumikia jukumu lolote ambalo atapewa ikiwa Bw. Kagame ataona inafaa.

“Kutoka ndani ya moyo wangu, naomba radhi kwa Rais wa Jamhuri na umma kwa ujumla,” aliandika.

"Ilikuwa makosa kwangu kuendesha gari nikiwa nimekunywa pombe. Nimeamua kuacha pombe" aliandika katika mtandao wake wa Twitter

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments