MANISPAA YA SHINYANGA YAKUTANA NA WADAU WA BIASHARA KUJADILI NAMNA YA KUKUZA MZUNGUKO WA KIFEDHA

 

Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura akizungumza kwenye kikao cha wadau wa biashara manispaa ya Shinynaga.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

MANISPAA ya Shinyanga imefanya kikao na wadau wa biashara, kujadili namna ya kukuza mzunguko wa kifedha katika Manispaa hiyo ili isongembele kimaendeleo na kukua kiuchumi.

Kikao hicho kimefanyika leo Oktoba 20, 2022 katika ukumbi wa manispaa hiyo kwa kukutanisha wafanyabiashara mbalimbali, pamoja na wawekezaji wa viwanda.

Akizungumza kwenye kikao Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura, amesema lengo la kikao hicho ni kuona Manispaa ya Shinyanga inasonga mbele kimaendeleo, kukuza mzunguko wa kifedha pamoja na kupaa kiuchumi.

Amesema manispaa ya Shinyanga imekuwa ikidumaa kimaendeleo sababu ya kuwapo na mzunguko wa kifedha, na hiyo inatokana na sababu mbalimbali ikiwamo na wafanyabiashara kupandisha bei juu za bidhaa, tofauti na maeneo mengine ikiwamo Kahama na Mwanza.

“Manispaa ya Shinyanga ndiyo Makao Makuu ya Mkoa wa Shinyanga, lakini maendeleo yake yana kwenda kwa kasi ndogo, moja ya sababu bei za bidhaa zipo juu sana, na kusababisha wananchi kukimbilia maeneo mengine kwenda kupata huduma na hatimaye mzunguko wa fedha kuwa chini,”amesema Satura.

“Mfano bidhaa ambazo zinauzwa hapa Shinyanga zipo juu sana ukilinganisha na Kahama, lakini wafanyabiashara hawa wanachukua mali sehemu moja, ndiyo maana Kahama inakuwa na mzunguko mkubwa wa kifedha sababu watu wengi wanakimbilia huko kupata mahitaji yao,”anaongeza.

Aidha, amewataka wafanyabiashara katika Manispaa hiyo wabadilike na kuuza bidhaa zao kwa bei ya kawaida, ili wananchi wasikimbilie maeneo mengine kwenda kupata mahitaji yao, bali wabaki hapo hapo Shinyanga na hatimaye kukuza mzunguko wa kifedha na kusonga mbele kimaendeleo.

Amesema kwa upande wa Serikali wameanza mikakati ya kurejesha heshima ya Manispaa ya Shinyanga kama makao Makuu ya Mkoa na kuwa kitovu cha biashara, kwa kuboresha miundombinu mbalimbali ya biashara, pamoja na kupandisha hadhi vyuo vya kati, viwe vyuo vikuu ili kuongeza idadi ya watu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kikao hicho Dk, Kulwa Meshack, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara Mkoa wa Shinyanga, amesema maendeleo ya eneo husika yanaletwa na wananchi wenyewe, na kutoa wito kwa wafanyabiashara hasa wa vifaa vya ujenzi wapunguze bei ya bidhaa zao.

Nao baadhi ya wafanyabiashara ambao wamehudhulia kikao hicho, wamesema tatizo la mfumuko wa bei za bidhaa katika Manispaa ya Shinyanga, linasababishwa na wafanyabiashara kufanya biashara kimazoea.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura akizungumza kwenye kikao cha wadau wa biashara Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara Mkoa wa Shinyanga Dk. Kulwa Meshack akizungumza kwenye kiao hicho cha wadau wa biashara Manispaa ya Shinyanga.

Kaimu Mchumi wa Manispaa ya Shinyanga Michael Makotwe akiwasilisha taarifa ya uelekeo wa Manispaa ya Shinyanga ifikapo mwaka 2025 kwenye kikao cha wafanyabiashara.

Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii Manispaa ya Shinyanga John Tesha. akiwasilisha taarifa ya kamati ya uhamasishaji wa ukusanyaji wa mapato kodi ya huduma.
Afisa Biashara wa Manispaa ya Shinyanga Mirembe George akiwasilisha mada ya urasimishaji wa biashara kwenye kikao hicho cha wadau wa biashara.

Wadau wa biashara wakiwa kwenye kikao cha majadiliano namna ya kuukuza mji wa Shinyanga kimaendeleo pamoja na kuongeza mzunguko wa kifedha.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.
Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.
Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.
Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Wadau wa biashara wakiendelea na kikao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments