SIMBA SC YAENDELEZA UBABE KIMATAIFA, YAICHAPA NYASA BIG BULLETS 2-0



**********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Simba imefanikiwa kutinga hatua inayofuata Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufanikiwa kuichapa Nyasa Big Bullets mabao 2-0 na kufikia jumla ya mabao 4-0 baada ya mechii ya kwanza Simba Sc akiwa ugenini kupata mabao 2-0.

Simba Sc imepata mabao kupitia kwa Moses Phiri ambaye amepachika mabao yote mawili na kuiwezesha timu yake kutinga hatua inayofuata Ligi ya Mabingwa Afrika.

Simba Sc inatinga hatua inafuata na kuungana na wenzake Yanga Sc ambao nao jana walifanikiwa kutinga hatua hiyo baada ya kuwachapa Zalan Fc kwa jumla ya mabao 9-0.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments