KINANA ATUA KIGOMA KWA ZIARA YA KUIMARISHA CHAMA

 


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Ndugu Abdulrahman Omari Kinana amewasili leo Alhamisi tarehe 01 Septemba, 2022 mkoani Kigoma kwa ziara ya siku moja mkoani humo ya kukagua uhai wa chama, utekelezaji wa ilani pamoja na kusikiliza kero za wananchi.


Kinana amewasili uwanja wa ndege wa Kigoma na kupokelewa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kigoma Ndg Amandus Dismas Nzamba, Mkuu wa mkoa wa Kigoma Ndg Thobias Andengenye, wanachama na viongozi  wa chama na serikali.

Kinana ameanza leo ziara ya siku moja mkoani Kigoma ambapo ataendelea katika mikoa ya Kagera, Geita na Mwanza. Katika ziara yake ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndg Shaka Hamdu Shaka.

#CCMImara
#KaziIendelee


 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments