WILLIAM RUTO AAPISHWA KUWA RAIS WA KENYA

William Ruto akila kiapo 
William Ruto ameapishwa rasmi kuwa rais wa tano wa Jamhuri ya Kenya leo Jumanne Septemba 13,2022 katika uwanja wa Moi Kasarani katika sherehe iliyosimamiwa na msajili Mkuu wa mahakama Anne Amadi mbele ya jaji mkuu Martha Koome.


“Mimi, William Samoei Ruto, kwa kutambua kikamilifu wito wa juu ninaochukua kama Rais wa Jamhuri ya Kenya, naapa kwamba nitakuwa mwaminifu wa kweli kwa Jamhuri ya Kenya", ameapa rais mpya William Ruto akiapishwa na Msajili Mkuu wa Mahakama Anne Amadi, mbele ya Jaji Mkuu Martha Koome.
Mkewe Mama Rachel Ruto alikuwa amesimama kando yake wakati akila kiapo hicho akishuhudiwa na zaidi ya wakuu 20 wa nchi mbalimbali.

Ruto mwenye umri wa miaka 55 amekula kiapo kwa kutumia nakala ya katiba ya Kenya, wiki tano baada ya uchaguzi wa Agosti 9, akichukua hatamu za nchi iliyokumbwa na ukame na mzozo wa gharama ya maisha.


Alitangazwa mshindi mnamo Agosti 15,2022 baada ya kumshinda kiongozi wa Upinzani wa muda mrefu Raila Odinga ambaye baadaye aliomba ushindi huo katika Mahakama ya Juu ambapo kesi hiyo ilitupiliwa mbali kwa kukosa ushahidi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments