RC MJEMA ASHUHUDIA UWEKAJI SAINI WA MIKATABA ZABUNI YA UJENZI WA BARABARA… "FEDHA ZIPO, MKAJENGE KWA WAKATI, VIWANGO"


Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa (kulia) akibadilishana Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga na Mkurugenzi wa Kampuni ya MIDA Women Group, Milka Marisham.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema, amesema hatakubali kuona utekelezaji mbovu wa ujenzi wa miradi ya maendeleo huku akiwataka Wakandarasi wanaojenga miundo mbinu ya barabara kujenga kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.


Dkt. Mjema amesema hayo leo Jumanne Septemba 6, 2022 wakati akishuhudia hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.


Wakandarasi hao watatu wazawa waliosaini Mkataba na TARURA ni MIDA Women Group, Joline Women Group na Corsyne Consult Ltd ambao watajenga barabara za kiwango cha changarawe na madaraja kwenye maeneo mbalimbali mkoani Shinyanga.


Dkt. Mjema amesema jumla ya shilingi Bilioni 2.6 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya barabara hivyo anachotaka ni ujenzi kufanyika kwa wakati na kwa kuzingatia ubora unaotakiwa.


“Fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara zipo, nendeni mkajenge barabara za viwango na mtekeleze kwa wakati uliopangwa. Tunataka barabara za viwango zitakazodumu kwa miaka 20 na siyo mwaka mmoja tu barabara inakuwa mbovu mnaanza kuzikarabati, hilo hatutaki. Ninyi ni wakandarasi wazawa fanyeni kazi zenu kwa ufanisi mkubwa na mshindane na Wakandarasi kutoka Nje ya nchi,”amesema Mjema.


“Tunataka kupokea barabara zenye viwango vya juu. Nategemea barabara zote ziwe na viwango. Hatutakubali kuona wala kupokea ujenzi wa barabara ambayo ipo chini ya kiwango,”ameongeza Mjema.


Kwa upande wake, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Ramadhani Masumbuko amesema amefurahi kuona Wakandarasi wazawa akibainisha kuwa kutokana na kwamba miundombinu ya barabara ni kiungo muhimu cha ukuaji wa uchumi ana imani kuwa Wakandarasi hao wazawa watatekeleza miradi hiyo kwa ufanisi mkubwa huku akiwataka TARURA kuwa makini kusimamia ujenzi wa miundo mbinu kwa hatua zote.

Naye Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa amesema kati ya bajeti iliyotengwa kwa Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya matengenezo ya barabara kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ni shilingi 15,321,240,000/= na kwamba mikataba hiyo iliyosainiwa ni ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha changalawe na madaraja katika wilaya za Kahama, Shinyanga na Kishapu.

“Nawapongeza Wakandarasi walioshinda zabuni hizi nawaasa watekeleze miradi hii kwa kuzingatia ubora na muda uliopangwa. Barabara hizi zikiboreshwa zitachochea sana ukuaji wa uchumi wa wananchi kwa mkoa wetu na kuboresha sana sekta za kilimo na utalii”,amesema Mhandisi Mlekwa.

Katika hatua nyingine amesema TARURA Mkoa wa Shinyanga inahudumia mtandao wa barabara wenye urefu wa Km 5,220.02, kati ya hizo barabara za lami ni Km 38.132, barabara za changarawe ni km 1,414.70 na barabara za udongo ni Km 3,767.19.

Nao Wakurugenzi wa Makampuni hayo ya Ukandarasi Flora Charles Gabba wa Kampuni ya Joline Women Group na Denis Kisoka wa Kampuni ya Corsyne Ltd na Milka Marisham wa Kampuni ya MIDA Women Group wameipongeza Serikali kwa kujali Wakandarasi wazawa na kuwapatia kazi ya ujenzi wa miundombinu ya barabara huku wakiahidi kutowaangusha na kutekeleza kazi zao kwa kiwango bora na kuikamilisha kwa wakati.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza leo Jumanne Septemba 6, 2022  katika ukumbi wa Chuo cha Ualimu Shinyanga (SHY COM) Mjini Shinyanga wakati akishuhudia hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza wakati akishuhudia hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6. 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza wakati akishuhudia hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6. 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema akizungumza wakati akishuhudia hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6. 
Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa akizungumza wakati wa hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya TARURA na Wakandarasi yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6. 
Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa akizungumza wakati wa hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya TARURA na Wakandarasi yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6. 
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhani Masumbuko akizungumza wakati wa hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya TARURA na Wakandarasi yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6. 
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Prof. Siza Tumbo akizungumza wakati wa hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya TARURA na Wakandarasi yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6. 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema (katikati) akizungumza wakati akishuhudia hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6. 
Afisa Sheria wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Shinyanga, Male Samson Mathias (kulia) akizungumza wakati wa hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya TARURA na Wakandarasi yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6. 
Mkurugenzi wa Kampuni ya MIDA Women Group, Milka Marisham akisaini Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga iliyosainiwa kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi.
Afisa Sheria wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA)Mkoa wa Shinyanga, Male Samson Mathias (mwenye suti nyeusi) na  Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa wakisaini Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga iliyosainiwa kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi.
Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa akisaini Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga iliyosainiwa kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi.
Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa (kulia) akibadilishana Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga na Mkurugenzi wa Kampuni ya MIDA Women Group, Milka Marisham.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Joline Women Group,  Flora Charles Gabba (kushoto) akisaini Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga iliyosainiwa kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Joline Women Group,  Flora Charles Gabba (kushoto) akisaini Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga iliyosainiwa kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi. Kulia ni Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa.
Zoezi la kusaini Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga iliyosainiwa kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi likiendelea.
Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa akisaini Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga iliyosainiwa kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi.
Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa (kulia) akibadilishana Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga na Mkurugenzi wa Kampuni ya Joline Women Group,  Flora Charles Gabba.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Corsyne Ltd, Denis Kisoka (kushoto) akisaini Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga iliyosainiwa kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi.
Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa akisaini Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga iliyosainiwa kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi.
Afisa Sheria wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA)Mkoa wa Shinyanga, Male Samson Mathias (mwenye suti nyeusi) akisaini Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga iliyosainiwa kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi.
Meneja Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) mkoa wa Shinyanga Mhandisi Oscar Gilbert Mlekwa (kulia) akibadilishana Mikataba ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga na Mkurugenzi wa Kampuni ya Corsyne Ltd, Denis Kisoka
Wadau wakiwa kwenye hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.
Wadau wakiwa kwenye hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.

Wadau wakiwa kwenye hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.
Wadau wakiwa kwenye hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.
Wadau wakiwa kwenye hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.
Wadau wakiwa kwenye hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.
Wadau wakiwa kwenye hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.
Wadau wakiwa kwenye hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.
Wadau wakiwa kwenye hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.
Wadau wakiwa kwenye hafla ya Usainishaji Mikataba 15 ya Zabuni ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na madaraja mkoa wa Shinyanga kati ya Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) na Wakandarasi watatu yenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.6.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments