WATUMISHI WA WILAYA YA TEMEKE WAMPONGEZA RAIS SAMIA KWENYE NYONGEZA YA MSHAHARA

Mtumishi wa Wilaya ya Temeke Bi.Makungu Shomari akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 wakati wakitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya. Mtumishi wa Wilaya ya Temeke Bi.Makungu Shomari akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 wakati wakitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya. Mtumishi wa Wilaya ya Temeke Bi.Makungu Shomari akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 wakati wakitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya. Baadhi ya watumishi wa Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 wakati wakitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya. Baadhi ya watumishi wa Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 wakati wakitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

*********************

Na Mwandishi wetu.

WATUMISHI wa kada mbalimbali katika Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam wamempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa juhudi ambazo anazifanya hasa kuwajali watumishi na kuzingatia maslahi yao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 Jijini Dar es Salaam,Mtumishi wa Wilaya ya Temeke Bi.Makungu Shomari amesema kuwa Rais Samia ndani ya kipindi chake cha muda mfupi ameweza kuleta nafuu na faraja kwa watumishi wa Umma.

"Kuhusu suala la nyongeza ya asilimia 23 sisi watumishi tumelielewa sana mana lengo kuu Rais Samia amezingatia kuboresha Hali za kiuchumi za watumishi wa kiwango cha chini ambao ni wengi zaidi katika kada mbalimbali za utumishi wa umma, hapa amezingatia wenye viwango vidogo vya mishahara". Amesema Bi.Makungu

Aidha amesema kuwa Rais Samia amejipambanua kuwa anawajali watumishi sana na kwa kuzingatia maslahi yao na alianza kwa kuwaondolea kadhia ya watumishi wenye deni la mkopo wa elimu ya juu,

"Rais Samia alipoingia madarakani alifuta penati hii na imeleta ahueeni kubwa na Sasa Deni linalipika, baada ya mabadiliko hayo aliyekuwa analipa milioni 8 Sasa analipa milioni 4 pekee."Amesema

Pamoja na hayo amesema kuwa suala la posho na nauli amesema Rais Samia ameongeza kiwango kwa asilimia 100 na hii imeleta ahueni kwa watumishi wanapopewa kazi maalumu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments