RAIS SAMIA AMTEUA ERIC HAMISSI KUWA MKURUGENZI WA MSCL, KAGAIGAI MWENYEKITI BODI YA TBC


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemteua, Eric Hamissi kuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) ambapo Kabla ya uteuzi huo Hamissi alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

Rais Samia pia amemteua Stephen Kagaigai kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Kagaigai anachukua nafasi ya Balozi Herbert Mrango ambaye amemaliza kipindi chake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments