RAILA ODINGA APINGA MATOKEO YA URAIS KENYA

Kiongozi wa Muungano wa Azimio nchini Kenya Raila Odinga amepinga matokeo ya uchaguzi uliomtangaza William Ruto kuwa ndiye Rais Mteule.


Raila amesema kwamba hakubaliani na matokeo hayo kwa sababu mwenyekiti wa tume hiyo alikiuka sheria ya tume hiyo kabla ya kumtangaza mshindi


Amesema kwamba makamishna wa tume hiyo hawakukubaliana kuhusu hesabu ya mwisho ya matokeo hayo yaliompatia ushindi William Ruto.


''Takwimu zilizotangazwa na Chebukati ni batili kwa maoni yetu, hakuna mshindi kisheria, aliyetangazwa kihalali wala rais mteule''.


Hata hivyo Raila amewasihi wafuasi wake kujizuia akiongezea kwamba atakwenda mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi huo.


''Jana, demokrasia yetu changa ilikumbwa na msukosuko mkubwa, kwa sababu hiyo, Kenya inakabiliwa na mgogoro mkubwa wa kisheria na kisiasa kutokana na matendo ya Wafula Chebukati''.


''Tunafuatilia njia za kisheria na za amani. Tuna hakika kwamba haki itatendeka. Tunaelewa kuwa ni Bw Chebukati pekee ndiye aliyepata kujumlisha kura za urais. Aliwanyima makamishna wote kupata taarifa hizo'', aliongeza Raila akizungumza na vyombo vya habari jijini Nairobi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments