WANAOSAIDIA OMBA OMBA JIJINI DAR ES SALAAM KUKAMATWA


Jiji la Dar es Salaam limepiga marufuku watu kuwasaidia ombaomba waliokithiri katika maeneo mbalimbali jijini humo huku hatua kali zikitangazwa kuchukuliwa kwa wanaoendelea kuwasaidia.


Akizungumza na EATV Meya wa Jiji la Dar es Salaam Omary Kumbilamoto, ambaye amesema kwamba, wameamua kuchukua uamuzi huo katika hatua za kuendelea kulipendezesha jiji la Dar es Salaam, huku akiwataka watu kwenda kutoa misaada kwenye maeneo maalum yaliyotengwa kudhibiti pia biashara haramu ya watu wanaowatumia watoto kuomba hela.


Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments