WAHADZABE WAPEWA NYUMBU 20 WASHIRIKI SENSA


Nyumbu

Wizara ya Maliasili kupitia Mkuu wa mkoa wa Manyara Makongoro Nyerere, imekabidhi Nyumbu zaidi ya 20 kwa wananchi jamii ya Wahadzabe eneo la Yaeda Chini wilayani Mbulu, ili kutekeleza ahadi ya kutoa nyama kwa jamii hiyo ili iweze kushiriki kikamilifu zoezi la Sensa.

Akikabidhi Nyumbu hao kwa jamii hiyo RC Nyerere amewaomba wananchi hao kujitokeza na kutoa ushirikiano wa kutosha katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi linaloendelea nchini.

Akipokea kwa niaba ya wananchi wa jamii ya Wahadzabe, kiongozi wa mila Athuman Magandula, ameishukuru serikali kwa kutekeleza ahadi hiyo.

Zoezi la Sensa nchini litaendelea kwa siku saba.

Via >> EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments