MWALIMU MKUU AANGUKA NA KUFARIKI AKIELEKEA SHULENI


Hali ya huzuni ilitanda katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Shitoto iliyoko Mumias Mashariki, Kaunti ya Kakamega baada ya mwalimu wao mkuu kuzirai na kufariki alipokuwa akielekea shuleni.


Akizungumza na moja ya vyombo vya habari ,mtoto wake Edgar Akwabi alisema marehemu Lily Mbati ambaye alikuwa na ugonjwa wakisukari alikuwa mzima usiku wa kuamkia jana.


"Nilizungumza na mama kwa simu na kumhimiza anywe dawa zake kama kawaida, na alinijibu kuwa atafanya hivo," Akwabi alisema.


Baadaye alipigiwa simu asubuhi na majirani waliomjulisha kuwa mama yake alianguka akielekea kazini na kufariki.


Naibu wa Mbati, Ruth Musafu kwa upande wake alimkumbuka marehemu bosi wake kama kiongozi wa kutegemewa, aliyejitolea na aliyependa kazi ya ualimu.


"Sote tutamkumbuka sana. Tunaomba neema huku tukimuomboleza mkuu wetu mpendwa," Musafu alisema.


Marehemu Mbati ndiye aliyekuwa mwalimu pekee wa somo ya Sayansi ya Nyumbani katika shule hiyo.


Taasisi hiyo imeitaka Wizara ya Elimu kuliangalia suala hilo wanapojiandaa na mitihani ya kitaifa.


Mwili wa marehemu ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhia aiti cha hospitali ya St Mary's.


Haya yanajiri baada ya kifo ya naibu ya mwalimu mkuu katika shule ya wasichana ya Migigo, ambapo mtoto wa marehemu mvulana aliuwa mamake katika hali isiyoeleweka.


Hii ikiwa ni kisa cha pili mwezi huu kuhusu vifo vya walimu kwa hali isi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments