DEREVA WA DALADALA MBARONI TUHUMA ZA KUUA KONDAKTA 'MPENZI WAKE'

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Maarifa Matala mwenye umri wa miaka 45, ambaye ni dereva wa daladala na mkazi wa Kimara kwa tuhuma za mauaji ya mtu aliyedaiwa kuwa mpenzi wake ambaye alikuwa ni kondakta.


Akizungumza Agosti 17, 2022, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Jumanne Muliro, amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa baada ya kutoroka na kukimbilia mkoani Lindi akidaiwa kumuua mpenzi wake aliyetambulika kwa jina la Sharifa ambaye alikuwa ni kondakta.


Aidha Muliro ameeleza kuwa katika hatua nyingine wamemkamata Gama Swai, anayetuhumiwa kwa kuuza spea za magari zinazodhaniwa kuwa vifaa vilivyoibwa kwenye magari ya wananchi.

Via >EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments