MREMBO AFARIKI KWA KUZAMA 'SWIMMING POOL' ...ALIKUWA ANAOGELEA HUKU AKIJIREKODI LIVE FACEBOOK


Mrembo Hellen Wendy aliyefia kwenye swimming pool nchini Canada
**
MREMBO raia wa Kenya aliyekuwa akifanya kazi ya uuguzi nchini Canada, Hellen Wendy amefariki dunia baada ya kuzama wakati akiwa anaogelea kwenye ‘swimming pool’.


Kabla hajafikwa na umauti, Hellen alikuwa akijirekodi ‘live video’ kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook, ambapo anaonekana kwenye video hiyo, akiwa anazungumza na marafiki zake kwenye mtandao huo.


Akiwa anaendelea kufurahi na marafiki zake huku akiogelea, ghafla Hellen alionekana akianza kutapatapa kwenye maji na akasikika akipiga mayowe ya kuomba msaada, kisha akazama.


Video aliyokuwa ameianzisha Facebook, iliendelea kuwa kwa takribani saa 3, huku ikionesha kwamba alifariki dunia dakika 10 au dakika ya 11 tangu alipoanza kurekodi video hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments