BABU WA MIAKA 92 AFAULU MTIHANI DARASA LA TANO KWA ALAMA ZA JUU ZAIDI

Mwanamume mkongwe wa miaka 92 anayeaminika kuwa mwanafunzi mzee zaidi nchini Uingereza kufanya mtihani wa GCSE amefaulu mtihani wake wa somo la hesabu darasa la tano – kwa alama ya juu zaidi.

Derek Skipper, kutoka Orwell huko Cambridgeshire, alifanya mtihani baada ya kusoma kupitia Zoom.

Mara ya mwisho alifanya mtihani wa hesabu mwaka wa 1946 alipotumia mfumo wa slaidi, lakini wakati huu alikuwa na kikokotoo na miwani ya kumwezesha kuona vizuri zaidi kwa sababu ya matatizo ya macho.

Alisema alifurahishwa na kupita mtihani huo.

Chanzo - BBC Swahili

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments