HAULE AONGEZA JOTO LA UCHAGUZI JUMUIYA YA WAZAZI

John Francis Haule

Ndivyo unavyo weza kusema wakati uchaguzi wa ndani ya CCM na jumuiya zake ukiendelea kuanzia ngazi ya matawi, kata, wilaya hadi taifa. Kijana John Francis Haule (MIAKA 37), Ambaye ni kada wa ccm na  mwkt wa jumuiya ya wzazi wa tawi la nala chinagali Dodoma, amejitosa katika kinyang’anyiro cha  nafasi ya mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi taifa.

Hayo yamejiri jana katika ofisi za wazazi taifa Jijini Dodoma wakati HAULE akirejesha  fomu yake ya kugombea nafasi hiyo  ndani ya jumuiya ya wazazi .

Akizungumza na mwandishi wa  Ngasa online tv Ndg Haule  alisema kuwa ameamua kuchukua fomu  na kurejesha katika nafasi hiyo kwa kuwa anamaini kuwa   ana uzoefu na nia ya dhati ya kuitumikia jumuiya hiyo na chama cha mapinduzi kwa ujumla wake. 


Kwa mujibu wa Haule  ambaye ni msomi wa shahada ya sayansi ya siasa na utawala  (POLITICAL SCIENCE AND PUBLIC ADMINISTRATION  DEGREE WITH HONOR. PSPA)  ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam.   


  Haule ambaye ni mzaliwa wa Ludewa mkoani Njombe akiwa mwanachama hai wa CCM kuwa anatia nia kugombea nafasi hiyo kwa mujibu wa katiba ya ccm na jumuiya ya wazazi inayo toa haki kwa kila mwanachama ya kuchagua na kuchaguliwa.

PONGEZI KWA RAIS NA MWKT WA CCM TAIFA MH: SAMIA SULUHU HASAN

Ndg Haule wakati akizungumza kupitia Ngasa on line TV.allitumia fursa hiyo kutoa pongezi za thati kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake mzuri unaozingatia mifumo yote ya demokrasia,kwa mujibu wa Haule  alibainisha kuwa  Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere  alipata kusema kuwa ili taifa lolote lipate maeendeleo linaitaji siasa safi na uongozi bora hivyo  Mhe. Samia Suluhu Hassan  ni mfuasi mahiri wa falsafa ya siasa safi nauongozi bora kama ilivyo wahi  bainishwa na BABA WA TAIFA.


 Pia Haule alisema kuwa  Mhe. Samia Suluhu Hassan ni kiigizo chema na ni mfano mzuri wa  kiongozi anayeongoza Taifa kwa kuongozwa na sheria nasio kuiongoza sheria,na pia katika  tawi la nala chinangali wana mwita kuwa  ni ‘Malkia wa siasa safi wa karne hii ya 21’

MAONO JUU YA CCM NA JUMUIYA YA WZAZI

 Kwa mujibu wa HAULE maono yake juu ya CCM na jumuiya ya wazazi ya mejikita katika kitabu cha TUJISAHIHISHE  1962 Kilicho andikwa na  Rais wa TANU J. K. NYERERE kikibainisha dhima ya ukweli kuwa hauna umri  na unatabia ya kujilipiza kiasi ukipuuzwa.


Katika hilo Ndg Haule  alisema kuwa  CCM inapaswa kufanya maboresho ya katiba ya CCM ya mwaka 1977 hususni katika kipengele cha mgombea urais kuwa rais  aliyoko madarakani anaye tokana na CCM ataendelea kwa kipindi kingine cha miaka mitano ndani ya CCM bila kushindana na mwanachama mwingine yeyote  ndani ya CCM.

 Ili kuweza kuepuka  dhana kwamba CCM ina tamaduni mana mwaka 2020  Ndg BERNAARD MEMBE alichalenge CCM Kuwa CCM haiongozwi na tamaduni bali inaongozwa na katiba, so that was a challenge aliongeza   Haule  na kusisitiza kuwa sasa niwakati muafafaka wa KUJISAHIHISHA kwa jambo hilo.

 Pia Haule alitoa ushauri kuwa  pia kuwepo na ukomo wa Umri wa viongozi waandamizi ndani ya jumuiya na chama kwa ujumla wake.

 “Endapo nitapata fursa ya kuwa Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi Taifa nitashauri suala la ukomo wa umri  kwa viongozi waandamizi wa jumuiya na chama liwekwe kwenye katiba ya jumuiya ya wazazi na CCM kwa ujumla wake”.

 UZOEFU NA UTUKMISHI NDANI YA CCM NA JUMUIYA ZAKE.

Kwa mujibu wa HAULE kuwa asha hudumu katika nafai mbalimbali ndani ya accm   kwa ujumla

1. 2022 Mwenyekiti wa  umoja wa wazazi Tawi la nala chinngali

2. Mjumbe wa mkutano mkuu UVCCM wilaya ya Ilala Dar es salaam

3.Mjumbe kamati ya fedha kata ya Ubungo Dar es salaam

4. Mjumbe kamati ya utekelezaji  umoja wa wzazi tawi la Abiyani chuo kikuu

5.katibu UVCCM/CCM tawi la chuo kikuu  (Abuyani  UDSM shirikisho la vyuo vikuu)

6.Mjumbe wa halimashauri kuu tawi la Mbuyuni  Tabata  Ilala

7.Mratibu na katibu wa makongamano ya shirikisho vyuo vikuu Dar es salaa

"Kwa uzoefu huu naamini  unatosha  kuiongoza jumuiya ya wazazi Tanzania",  aliongeza Haule.

 

USIMAMIZI WA MIRADI YA JUMUIYA YA WAZAZI

  Jumuiya ya wazazi dhima yake kuu ni kupambana dhidi ya ujinga hivyo moja kati ya miradi ya jumuiya  ni mashule yanayojulikana kama shule za wazazi , ambayo kwa kiasi kikubwa yamesaidia sana   katika kuondoa adui  ujinga.

"Hata mimi mwenyewe ni zao la shule ya wazazi  ambayo ni Ludewa Sekondari iliyoko mkoani Njombe  wilayani Ludewa. Kwa kutambua umuhimu huo nikiwa mwenyekit nitatoa msukumo wa  kasi ili kuziboresha Zaidi  kimiundo mbinu, mfumo wa utawala  pamoja na namana ya ueendeshaji ili ziweze kueendelea kuwa kinara katikaka tasinia ya elimu TANZANIA.

>Pia kuanzisha    miradi mingine ya jumuiya kama vile ujenzi wa vituo vya afya vijijini(VILLAGE MEDICS) Vyuo vya ufundi  shabaha nikueendelea kuipiga jeki serikali katika azma yake ya kuendeleaa  kuboresha maeendeleo ya nchi yetu na watanzania kwa ujumla.

 

 

 

 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments