MAFUNZO YA WALIMU NA WASIMAMIZI WA SENSA YAFUNGWA SHINYANGA… RC MJEMA ASISITIZA UZALENDO ‘MSIENDE NA YA KWENU”


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akizungumza wakati akifunga mafunzo ya Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga leo Jumatatu Julai 25,2022 katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu SHY COM Mjini Shinyanga yakihusisha washiriki 194. Picha na Kadama Malunde  - Malunde 1 blog


Na Kadama Malunde  - Malunde 1 blog

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema amefunga mafunzo ya Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga huku akiwasisitiza wahitimu hao wa mafunzo kuwa wazalendo na kuepuka kuwa wakali kwa wananchi.


Mafunzo hayo yaliyodumu kwa siku 21,2022 yamefungwa leo katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu SHY COM Mjini Shinyanga yakihusisha washiriki 194.


“Nendeni  mkamalize kazi, kafundisheni yale mliyofundishwa. Msiende kupotosha jamii kuhusu sensa ya watu na makazi, nendeni mkafanye kazi kwa uzalendo na umakini mkubwa ili sensa ya watu na makazi iwe na mafanikio”,amesema Mjema.


“Msiende na ya kwenu,nendeni mkatumie madodoso mliyofundishwa. Muwe wapole mnapoongea na wananchi. Usiwe mkali kama mwananchi hafunguki unapomuuliza”,ameongeza Mjema.


Ametumia fursa hiyo kuwataka viongozi na wadau mbalimbali kuendelea kutoa elimu ya sensa ya watu na makazi huku akibainisha kuwa mkoa wa Shinyanga umejipanga kikamilifu kufanikisha zoezi  la sensa ya watu na makazi Agosti 23,2022.


“Kazi iliyobaki sasa ni kulipiga debe la sensa hadi kieleweke. Ukiwa na mkeo  au mmeo huko nyumbani mwambie kuhusu Sensa, tuongeze juhudi za kutoa elimu ya sensa na makazi”,amesema.


Mratibu wa Sensa ya Watu na Makazi Mkoa wa Shinyanga,  Eliud Kamendu amesema mafunzo ya Makarani, Wasimamizi wa Maudhui na wasimamizi wa TEHAMA mkoa wa Shinyanga  yaliyofanyika kwa siku 21 yalianza Julai 6,2022 na yatafikia tamati Julai 26,2022 yakiwa na jumla ya washiriki 194 kati yao makarani 184, wakufunzi 7, mratibu msaidizi wa sense mkoa na mratibu wa sensa mkoa.


“Mafunzo haya yalianza kutolewa kwa kufundisha Dodoso la Jamii, Dodoso kuu la sense, dodoso la makundi maalumu, dodoso la majengo na miongozo mbalimbali ya wakufunzi, wadhibiti ubora na waratibu wa sensa ngazi ya wilaya. Hali kadhalika mafunzo haya yalijumuisha kwenda uwandani kujifunza kwa vitendo mambo yote yaliyofundishwa darasani katika madodoso yote sambamba na kufanya majaribio kwa makarani”,amesema Kamendu.


“Mafunzo haya yamefanyika katika ubora wa hali ya juu na timu hii imekuwa timu ya ushindi ambayo itakwenda kuwafundisha vyema makarani, wasimamizi wa maudhui na wasimamizi wa TEHAMA ngazi ya wilaya kuanzia Julai 29,2022 hadi Agosti 16,2022 kwa ustadi mkubwa ambao ndiyo watakaokwenda kutekeleza zoezi zima la sensa ya watu na makazi kwa mwaka 2022”,ameeleza Kamendu.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akizungumza wakati akifunga mafunzo ya Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga leo Jumatatu Julai 25,2022 katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu SHY COM Mjini Shinyanga yakihusishwa washiriki 194.  Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akizungumza wakati akifunga mafunzo ya Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga leo Jumatatu Julai 25,2022 katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu SHY COM Mjini Shinyanga yakihusisha washiriki 194. 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akizungumza wakati akifunga mafunzo ya Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga leo Jumatatu Julai 25,2022 katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu SHY COM Mjini Shinyanga yakihusisha washiriki 194. 
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bi. Zuwena Omary akizungumza wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akifunga mafunzo ya Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga leo Jumatatu Julai 25,2022 katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu SHY COM Mjini Shinyanga yakihusisha washiriki 194. Kulia ni Mstahiki Meya wa Manispaa  ya Shinyanga , Elias Masumbuko, kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Sophia Mjema.
 Mratibu wa Sensa ya Watu na Makazi Mkoa wa Shinyanga,  Eliud Kamendu akitoa taarifa ya mafunzo wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akifunga mafunzo ya Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga leo Jumatatu Julai 25,2022 katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu SHY COM Mjini Shinyanga.
Mratibu wa Sensa ya Watu na Makazi Mkoa wa Shinyanga,  Eliud Kamendu akitoa taarifa ya mafunzo wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akifunga mafunzo ya Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga leo Jumatatu Julai 25,2022 katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu SHY COM Mjini Shinyanga.
Katibu wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, Raphael Nyandi akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Mjema akifunga mafunzo ya Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga leo Jumatatu Julai 25,2022 katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu SHY COM Mjini Shinyanga.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.

Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi mbalimbali wakiwa ukumbini
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.

Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Viongozi mbalimbali pamoja na Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.
Walimu wa Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

1/Post a Comment/Comments

إرسال تعليق