BASI LA SHULE LAUA WATU 10 WAKIWEMO WANAFUNZI 8 ..RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA POLE

Ajali ya basi
Rais Samia Suluhu Hassan, ametuma salamu za pole kufuatia basi la wanafunzi wa Shule ya King David Mtwara lenye namba za usajili T 207 CTS lililopata ajali asubuhi ya leo Jumanne, Julai 26, 2022 eneo la Mikindani Mtwara likiwa na wanafunzi na kuua watu 10 wakiwemo wanafunzi nane wa shule hiyo.


Kamanda wa Polisi Mtwara Nicodemus Katembo amesema Wanafunzi waliofariki dunia ni wanane, Dereva mmoja na Mwangalizi mmoja, majeruhi ni 19.


Kupitia akaunti yake ya Twitter, Rais Samia ameandika: “Nimesikitishwa na vifo vya wanafunzi 8 wa Shule ya Msingi ya King David na watu wazima 2 vilivyotokea leo asubuhi huko Mtwara Mikindani baada ya gari la shule kutumbukia shimoni. Nawapa pole wafiwa, mkuu wa mkoa na jamaa. Mwenyezi Mungu awarehemu marehemu na kuwaponya majeruhi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments