ASKOFU MERY MUTAFUNGWA AWATAKA WANANCHI KUJIEPUSHA NA MAMBO YA UOVU SIKUKUU YA PASAKA

Askofu wa Makanisa ya Mlima wa Bwana Tanzania Mery Mutafungwa akihubiri wakati wa Ibada ya usiku wa mkesha wa Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Mlima wa Bwana Tanzania lililopo katika Kata ya Kashai Mtaa wa Kilimahewa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.

Na Mbuke Shilagi Kagera.
Askofu wa Makanisa ya Mlima wa Bwana Tanzania Mery Mutafungwa amewataka wananchi wote wanaposherehekea sikukuu ya Pasaka kujiepusha na mambo ya uovu.

Ameyasema hayo wakati wa Ibada ya usiku wa mkesha wa Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Mlima wa Bwana Tanzania lililopo katika Kata ya Kashai Mtaa wa Kilimahewa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.

Askofu Mery amesema kuwa watu wote wanatakiwa kujiepusha na mambo ya uovu pamoja na makundi mabaya katika kipindi hiki cha sikukuu.

Askofu Mery Mutafungwa ameongeza kuwa Sherehe ya Pasaka ni kumbukumbu ya Ufufuko wa Mkombozi wa Ulimwengu Yesu Kristo hivyo watu wanaposherehekea wanatakiwa kusherehekea kwa utulivu na amani kwa kufanya matendo mema na yakumpendeza Mungu.

Amewataka watu wote kuendelea kufanya yale matendo mema ambayo walitenda wakati  Kwaresma na kwamba imekuwepo watu wanapo maliza mfungo wa Kwaresma wanasahau kuendelea na unyenyekevu badala yake wanakuwa na matendo ya yasiyompendeza Mungu.

Ametoa wito kwa wazazi wanap toka na watoto kuelekea katika fukwe za ziwa kuwa na uangalizi mkubwa kwa watoto hao ili kuondoa usumbufu kwa Jeshi la Polisi na kwamba wanapokuwa makini na uangalizi mzuri kwa watoto wanapunguza usumbufu kwa jeshi la polisi pamoja na madhara yanayojitokeza.
Askofu wa Makanisa ya Mlima wa Bwana Tanzania Mery Mutafungwa akihubiri wakati wa Ibada ya usiku wa mkesha wa Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Mlima wa Bwana Tanzania lililopo katika Kata ya Kashai Mtaa wa Kilimahewa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.
Askofu wa Makanisa ya Mlima wa Bwana Tanzania Mery Mutafungwa akihubiri wakati wa Ibada ya usiku wa mkesha wa Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Mlima wa Bwana Tanzania lililopo katika Kata ya Kashai Mtaa wa Kilimahewa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera.
Kushoto ni Mchungaji msaidizi wa Kanisa la Mlima wa Bwana Tanzania lililopo kata ya Kashai mtaa wa Kilimahewa Mch. Frenk Thomas
Kulia ni Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Bwana Tanzania lililopo Kemondo Bukoba vijijini Mch. Seperatus Kashasha
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Mlima wa Bwana Tanzania lililopo kata ya Kashai mtaa wa Kilimahewa Mch.Fransisco Felician akizungumza kanisani
Baadhi ya waumini wa Mlima wa Bwana Tanzania waliohudhuria Ibada ya usiku ya Pasaka

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments