YANGA HAISHIKIKI NBC PREMIER LEAGUE, YAICHAPA GEITA GOLD 1-0



************************

NA EMMANUEL MBATILO


KLABU ya Yanga imeendelea kuusogelea ubingwa wa ligi ya NBC mara baada ya leo kuichapa Geita Gold 1-0 kwenye dimba la CCM Kirumba Jijini Mwanza.


Fiston Mayele ameendelea kuwatesa makipa wa ligi kuu ambapo leo tena kaweka kambani goli la pekee lililowapa pointi tatu muhimu kwenye ligi hiyo.


Mayele alifunga bao la mapema kabisa baada ya kuwashinda mabeki wa Geita Gold na kuweza kukwanjuka shuti kali lililomshinda kipa wa Geita Gold.


Mechi hii ambayo ilikumbwa na faulo nyingi kwa pande zote mbili na kusababisha wachezaji baadhi kutolewa nje kwa majeruhi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments