YANGA YAICHAPA MBAO FC BAO 1-0, YATINGA HATUA INAYOFUATA KOMBE LA ASF


*************************

NA EMMANUEL MBATILO,

KLABU Yanga imefanikia kusonga mbele hatua inayofuata mara baada ya kufanikiwa kuiondoa Mbao Fc kwa kuwanyuka bao 1-0 katika dimba la CCM Kirumba Jijini Mwanza leo hii.

Bao pekee la Yanga Sc liliwekwa kimyani na Mshambuliaji wao hatari Fiston Mayele ambaye alimalizia krosi iliyopigwa na Farid Mussa na kuweza kupachika bao kwa kichwa kilichoomshinda kipa wa Mbao Fc na kutinga nyavuni.

Kipindi cha kwanza milango yote ilikuwa migumu kwani mechi ilikwendaa mapumziko kwa timu zote mbili zikiwa hazijapata bao.

Kesho mahasimu wao Simba Sc watashuka dimbani kumenyana na Dar City katika dimba la Benjamin Mkapa .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments