JAMAA AVUNJIKA MIGUU YOTE KWA KUKANYAGWA NA TRENI ALIVYORUKA AKIKWEPA KUOMBWA NAULI


Jamaa mmoja amemalizia safari yake ya mwaka 2021 katika Hospitali ya Murang'a baada ya kuruka kutoka kwenye treni ya mizigo akihepa kukamatwa.

Mwanaume huyo mwenye umri wa kati aliruka kutoka kwenye gari la moshi la Nairobi-Murang'a katika eneo la Githurai, kaunti ya Kiambu mnamo Alhamisi, Disemba 30,2021 akihepa kulipa nauli ya KSh250 sawa na shilingi 5,250 za Tanzania zilizotozwa na matatu.

Safari yake ilianza vyema hadi alipofika Maragua na kuamua kuruka lakini alianguka kwenye barabara ya reli na kukanyagwa miguu na garimoshi hilo.

"Alihofia kwamba angekamatwa katika eneo la kituo cha mji wa Maragua. Hakupata hesabu kwa kuwa hakuweza kuruka kutoka kwenye treni na reli," alisema mkuu wa polisi katika kaunti ndogo ya Murang'a Kusini Alexander Shikondi.

Shikondi aliwaambia wandishi wa habari kuwa jamaa huyo aliokolewa na Wasamaria wema ambao walimpeleka hospitalini ambapo madaktari walipendekeza akatwe miguu yote.

"Tumefahamishwa na madaktari kuwa amepoteza miguu hiyo miwili. Madaktari wamekatwa vijiti ili kudhibiti majeraha," alisema. 

Mkuu huyo wa polisi alisema wakati waliwafahamisha maafisa wa Shirika la Reli la Kenya katika kituo cha Maragua, walisema hawafahamun tukio hilo na kila mmoja aliyeabiri treni hiyo yuko salama.

Chanzo- Tuko news

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments