Jeshi la Uganda lafanya mashambulio ya anga dhidi ya waasi wa ADF huko DRC
الثلاثاء, نوفمبر 30, 2021
Jeshi la Uganda limeanzisha mashambulizi ya pamoja ya anga na ardhini dhidi ya kundi la waasi la Allied Democratic Forces -ADF, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Uganda Brigedia Jenerali Flavia Byekwaso amethibitisha hayo kupitia akaunti yake rasmi ya twitter.
Alisema kuwa operesheni hizo zilifanywa na washirika wa Congo, dhidi ya kambi za ADF, lakini hakutoa maelezo zaidi kuhusu maeneo ambayo mashambulizi hayo yamefanywa.
Mamlaka ya Uganda inalaumu ADF, ambayo inashirikiana na Islamic State (IS) kwa msururu wa mashambulizi ya mabomu nchini humo tangu Oktoba.
Wiki mbili zilizopita, IS ilidai kuhusika na milipuko miwili ya mabomu nje kidogo ya Kituo Kikuu cha Polisi cha Kampala na karibu na Bunge.
Takriban watu watano wameuawa katika milipuko hii ya mabomu, baadhi ya mashambulizi yakiwa ya kujitoa mhanga, kwa mujibu wa Polisi wa Uganda.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin