Picha : MAHAFALI YA 23 YA SHULE YA SEKONDARI DON BOSCO DIDIA YAFANYIKA...WAZAZI WAKUMBUSHWA WAJIBU WAO

Wahitimu  wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga wakiwa katika picha pamoja.

Na Josephine Charles - Shinyanga 

Wazazi na Walezi wametakiwa kutekeleza Wajibu wao wa malezi ili kuepusha watoto wasijiingize katika matendo yasiyofaa kwenye jamii.

Hayo yamesemwa Oktoba 30,2021 na Katibu Tawala wa Wilaya ya Shinyanga bw. Boniphace Chambi kwenye mahafali ya 23 ya Shule ya Sekondari Don Bosco iliyopo Didia katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.

Katibu Tawala huyo ametolea mfano kipindi cha Corona wanafunzi walipoenda likizo baadhi yao walipata ujauzito,hiyo ikiwa inamaanisha kwamba kipindi walivyokuwa nyumbani wazazi hawakuzingatia nafasi zao katika malezi.

Katika risala aliyoisoma Mkuu wa Shule hiyo Fr. Felix Wagi amesema wanafunzi walioanza kidato cha awali mwaka 2017 Walikuwa ni wanafunzi 250 ambapo wasichana walikuwa 96 na wavulana 154 na waliohitimu kidato cha nne mwaka huu ni 164 kati yao wavulana ni 97 na wasichana ni 67 na kueleza kuwa upungufu huo umetokana na changamoto mbalimbali zisizozuilika.

Mkuu huyo wa Shule amesema mbali na mafanikio waliyopata tangu shule hiyo kuanzishwa mwaka 1994 baadhi ya changamoto walizonazo mpaka sasa ni pamoja na uhaba wa maji safi na salama kwa wanafunzi na upungufu wa mabweni.

Tazama picha hapa chini


Katibu Tawala wa Wilaya ya Shinyanga bw. Boniphace Chambi akizungumza kwenye mahafali ya 23 ya Shule Sekondari Don Bosco-Didia-Shinyanga
Katibu Tawala wa Wilaya ya Shinyanga bw. Boniphace Chambi akizungumza kwenye mahafali ya 23 ya Shule Sekondari Don Bosco-Didia-Shinyanga
Mgeni Rasmi Katibu Tawala wa Wilaya ya Shinyanga bw. Boniphace Chambia(katikati) akiwa na wageni waalikwa kushoto ni Mkurugenzi wa Gvenwear bi. Grace Mng'ong'o,kushoto mwenye skafu ni Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Jimbo katoliki Shinyanga pamoja na Mkurugenzi wa Radio Faraja Shinyanga Padre Anatoly Salawa pamoja na Uongozi wa shule ya Shule Sekondari Don Bosco-Didia-Shinyanga wa Kulia asiye na Skafu ni Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari Don Bosco Padre Vicent Mokaya,nyuma mwenye shati nyeupe ni Padre Kenneth Omondi na mwenye suti ni Mkuu wa Shule hiyo Padre. Felix Wagi wakiwa tayari kuelekea ukumbuni kunapofanyika mahafali ya 23 ya shule ya sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga.
Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga Padre Vicent Mokaya akizungumza kwenye mahafali ya 23 ya kidato cha 4 ya Shule hiyo
Mkuu wa Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga Padre Felix Wagi akizungumza kwenye mahafali ya 23 ya kidato cha 4 ya Shule hiyo
Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la TVMC lenye makao makuu yake Shinyanga bw. Musa Ngangala akizungumza kwenye mahafali ya 23 ya kidato cha 4 ya Shule hiyo
Mkurugenzi wa Kampuni ya Ushonaji na Ubunifu wa Mavazi iitwayo GVENWEAR iliyopo Shinyanga bi. Grace Mng'ong'o akizungumza kwenye mahafali ya 23 ya kidato cha 4 ya Shule hiyo
Mwandishi wa habari na Mtangazaji wa Radio Faraja 91.3 iliyopo Shinyanga ambaye pia ni balozi wa Don Bosco Sekondari Didia na Balozi wa Gvenwear bi. Josephine Charles akizungumza kwa niaba ya waandishi wenzake alioongozana nao kwenye mahafali ya 23 ya Shule hiyo.
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Jimbo katoliki Shinyanga pamoja na Mkurugenzi wa Radio Faraja Shinyanga Padre Anatoly Salawa akizungumza kwenye mahafali ya 23 ya Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga.
Makamu mkuu wa shule ya sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga Sister Mary Magdalene Mativo akizungumza kwenye mahafali ya 23 ya Shule hiyo.
Mtawala wa Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga Padre Kenneth Omondi akizungumza kwenye mahafali hayo.
Mgeni Rasmi pamoja na baadhi ya wageni waalikwa wakiwa tayari kwa ajili ya zoezi la ugawaji vyeti kwa wahitimu 164 wa kidato cha 4 Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga ikiwa ni mahafali ya 23 tangu shule hiyo kuanzishwa mwaka 1994.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Ushonaji na Ubunifu wa Mavazi iitwayo GVENWEAR iliyopo Shinyanga bi. Grace Mng'ong'o na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Jimbo katoliki Shinyanga pamoja na Mkurugenzi wa Radio Faraja Shinyanga Padre Anatoly Salawa wakiwa wamesimama Ukumbini kumsubiri Mgeni Rasmi amalize kusaini kitabu cha Wageni ndipo waketi.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Ushonaji na Ubunifu wa Mavazi iitwayo GVENWEAR iliyopo Shinyanga bi. Grace Mng'ong'o na Katibu Tawala wa Wilaya ya Shinyanga bw. Boniphace Chambi wakiwa wameketi ukumbuni kunapofanyika mahafali ya 23 ya Shule ya Sekondari Don Bosco-Didia.
Wageni waalikwa,Waalimu,Wazazi,Wahitimu na Wanafunzi wakiwa ukumbini kufuatilia matukio yanayoendelea kwenye mahafali ya 23 ya Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga.
Mgeni Rasmi,Wageni waalikwa,Waalimu,Wazazi,Wahitimu na Wanafunzi wakiwa ukumbini kufuatilia matukio yanayoendelea kwenye mahafali ya 23 ya Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga.
Mgeni Rasmi,Wageni waalikwa,Waalimu,Wazazi,Wahitimu na Wanafunzi wakiwa ukumbini kufuatilia matukio yanayoendelea kwenye mahafali ya 23 ya Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga.
Mgeni Rasmi,Wageni waalikwa,Waalimu,Wazazi,Wahitimu na Wanafunzi wakiwa ukumbini kufuatilia matukio yanayoendelea kwenye mahafali ya 23 ya Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga.
Mgeni Rasmi,Wageni waalikwa,Waalimu,Wazazi,Wahitimu na Wanafunzi wakiwa ukumbini kufuatilia matukio yanayoendelea kwenye mahafali ya 23 ya Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga.
Wahitimu 164 wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga wakijiandaa kutoa burudani ya wimbo mbele ya Mgeni Rasmi,Wageni waalikwa,Waalimu,Wazazi,Wahitimu na Wanafunzi wasiowahitimu.
Wahitimu 164 wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga wakiwa katika picha pamoja.
Wahitimu 164 wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga wakiwa katika picha pamoja na Mgeni Rasmi pamoja Wageni waalikwa katika mahafali ya 23 ya shule hiyo.
Wahitimu wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Don Bosco Didia-Shinyanga wakiwa wanafuatilia matukio ya burudani zinazoendelea kwenye mahafali ya 23 ya shule hiyo.

Picha zote na Josepine Charles & Kasisi Kosta

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments