MWANA FA AELEZEA AJALI ALIYOPATA


Mbunge wa jimbo la Muheza Hamis Mwinjuma maarufu Mwana FA
***
Mbunge wa jimbo la Muheza Hamis Mwinjuma maarufu Mwana FA, amepata ajali ya gari eneo la Mkambalani mkoani Morogoro jana Agosti 31, 2021 usiku.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Fortunatus Muslim na kueleza kuwa mbunge huyo yupo salama.

Kwa upande wake Mwana FA alipopata nafasi ya kuongea na waandishi wa habari alieleza kuwa kabla ya ajali waliona gari mbele yao inataka kupita gari (Overtake) na ilikuwa mwendokasi sana hivyo hawakuweza kuikwepa ndio ikawaparamia.

Picha kutoka eneo la ajali

Aidha amesema kiafya yeye na mwenzake aliyekuwa naye kwenye gari ni wazima ila alikuwa anasikia maumivu kidogo kifuani mwake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments