Na Munir Shemweta, MOROGORO
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amelitaka Shirika la Nyumba la Tifa (NHC) mkoa wa Morogoro kubuni miradi mipya ya ujenzi wa katika mkoa huo ili kuliwezesha shirika kuingiza fedha badala ya kutegemea nyumba za zamani.
Dkt Mabula alitoa kauli hiyo jana mkoani Morogoro wakati akizingumza na watumishi wa ofisi ya shirika hilo mkoa wa Morogoro akiwa katika ziara yake ya kusikiliza na kuzitafutia ufumbuzi kero za ardhi katika mkoa huo.
Alisema haileti maana NHC kutegemea nyumba zake zilizojengwa na mkoloni bila ya kuwa na mipango mipya ya ujenzi itakayowezesha shirika hilo kuwa na nyumba nyingine za kisasa zitakazoliwezesha shirika kujiongezea kipato.
Kwa mujibu wa Dkt Mabula, mkoa wa Morogoro bado una uhitaji mkubwa wa nyumba zikiwemo zile za kupangisha hasa kwenye maeneo mapya na kusisitiza kuwa NHC haina budi kuongeza kasi kwa kubuni miradi mipya itakayosaidia shirika kuongeza kipato.
‘’Kumbe ninyi bado mkoa kizamani yaani hamna mradi wa ujenzi wa nyumba mpya na mnategemea zile za zamani? Mnatakiwa kujiongeza kwa kubuni miradi mipya ili muweze kuongeza mapato ya shirika’’ alisema Dkt Mabula.
Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Mabula alimtaka Meneja wa NHC Morogoro Constantine Yuda kwenda katika halmashauri za mkoa huo ili kupatiwa maeneo kwa ajili ya ujenzi wa miradi mipya ikiwemo ya nyumba za watumishi kwenye halmashauri za mkoa huo.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin