Serikali kupitia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) wameahidi kuendelea kuunga mkono kazi mbalimbali za sanaa hapa nchini.
Hayo yamesememwa leo jijini Dar es Salaam na Afisa Sanaa Mwandamizi toka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Abel Ndaga wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya utoaji wa tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali.
“Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wenye zamana na Sekta ya Sanaa kupitia BASATA tutaendelea kutoa ushirikiano na wasanii mbalimbali ili kuweza kufanikisha malengo ya kukuza sekta ya sanaa nchini.
Afisa Sanaa Mwandamizi Ndaga ameongeza kuwa kuelekea siku ya utoaji tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali wanataraji kuwa tuzo hizo zitakuwa zitatoa hamasa kwa vijana wengi hapa nchini.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya utoaji tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali Joseph Ndalu ameahidi kuwa tuzo hizo zitaweka historia kwa kushirikisha wasanii wa tansia mbalimbali.
“Katika tuzo hizi tunatarajia kuwa na wasanii wa tasnia mbalimbali kama wasanii wafilamu, bongo fleva na sanaa mbalimbali hivyo ni imani yangu tuzo hizi zitakuwa za kipekee sana”alisema Bw. Ndalu.
Tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali zitafanyika siku ya jumamosi Juai tatu katika Kituo cha Mikutano Cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam kuanzia saa moja jioni.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin