JAMAA MGONJWA ATIMULIWA HOSPITALI BAADA YA KUMSHIKA NESI MAKALIO

Jamaa aliyekuwa akipokea matibabu katika hospitali moja eneo la Chogoria nchini Kenya amefukuzwa wodini kabla ya kupata nafuu baada ya kushindwa kula kwa macho akaishia kunyoosha mkono na kumgusa makalio nesi mkuu.

 Inasemekena ilikuwa ni mwendo wa saa mbili usiku ambapo wagonjwa wote walikuwa wamekula wakati nesi aliyekuwa zamuni alipita katikati ya wagonjwa katika wodi kuhakikisha kila mgonjwa anashughulikiwa.

Kwa mujibu wa Taifa leo, nesi huyo alikuwa amevalia sketi fupi mno bila kujali wagonjwa.

 Duru zinaarifu kuwa alipofika alikokuwa jamaa aligundua kuwa kulikuwa na mgonjwa kando yake aliyehitaji msaada. 

Alimuonesha jamaa mgongo kisha akaninama na kufaraghua sehemu yake ya nyuma iliyompagawisha na kumzuzua jamaa. Jamaa alipoona hivyo, akili zilimsimama akawaza na kuibuka na mawazo ya kumgusa nesi bila kujali matokeo yake.

“Samahani dada. Nimeshindwa kuvumilia urembo wako nikaona ni bora niguse,” jamaa mgonjwa alisema. 

“Mjinga wewe! Umefaidi nini? Nyie nyinyi vibaka tunaoogopa usiku. Watakaje?” Nesi aliuliza.

 “Niwie radhi dada. Samahani sitarudia tena,” jamaa alizidi kujitetea.

 “Kesho utaenda nyumbani kwa maana inaonekana haufai kuwa humu wodini. Wewe ni hatari kwa wagonjwa wengine na wafanyakazi katika hospitali hii,” muuguzi mkuu alimwambia jamaa

. Siku iliyofuata mapema asubuhi, jamaa aliamuriwa kuondoka hospitalini, japo hakuwa amepona na jamaa zake walipouliza ni kwa nini waliachwa vinywa wazi walipoarifiwa kuhusu alichomfanyia nesi mkuu usiku uliotangulia. 

“Huyu ni mtu hatari kuendelea kubaki katika wodi kwa sababu anaweza kuwadhuru wagonjwa na wafanyakazi. Tamaa yake imevuka mipaka. Ondokeni naye mkamuuguze nyumbani,” waliarifiwa.

 Penyenye zinasema kuwa baadhi yao walitishia kuishtaki hospitali kwa kumfukuza mgonjwa kabla ya kupona lakini naye nesi akawaambia angemshtaki kwa kumdhulumu kimapenzi.

Jamaa hakuwa na lingine ila kuchechemea akiondoka hospitalini humo, haikubainika iwapo jamaa zake walimpeleka hospitali nyingine

Chanzo - Tuko News

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments