KATIBU WA CHAMA CHA WASIOAMINI UWEPO WA MUNGU AJIUZULU

Chama cha Wasioamini Uwepo wa Mungu Nchini Kenya (AKS) kimepata pigo kubwa kufuatia kujiuzulu kwa katibu wao Seth Mahiga baada ya kuhudumu kwa mwaka mmoja unusu.

Mahiga amejiuzulu kutoka kwa wadhifa wake akisema amekutana na Yesu na hataki tena kuendelea kupiga kampeni za kumkana Mungu nchini.

Katika taarifa Jumamosi, Mei 29, 2021 rais wa chama hicho Harrison Mumia, alimtaja kama kiongozi aliyekuwa amejitolea mhanga na kumtakia kila la heri katika uhusiano wake mpya na Yesu Kristu.

"Tunamtakia Seth kila la heri katika uhusiano wake mpya na Yesu Kristu, tunamshukuru kwa kutumika chama hiki na bidii kwa zaidi ya mwaka mmoja unusu," ilisoma taarifa hiyo.

Chama hicho pia kilitangaza kuwa kiti hicho ki wazi na kuwaalika Wakenya kutuma maombi.

Chama hicho kilitangaza kuwa kiti hicho ki wazi na kuwaalika Wakenya kutuma maombi.

Kujiuzulu kwa Mahiga kulizua hisia mseto mtandaoni huku wanamtandao wengi wakimupa kongole kwa hatua hiyo.

Baadhi walimuhimiza Mumia kufuata mkondo huo wa mwangaza. Hii hapa baadhi ya maoni ambayo TUKO.co.ke imekuchagulia. Jaji Mkuu wa zamani Willy Mutunga alisema: "Rais.Endapo unategemea tu kipengee cha 32(1) cha katiba ambacho kinasema kila mtu ana haki ya kuabudu, dini, mawazo, imani na maono. Haki hii si ya kuchezea."

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments