Mkazi wa Mbagala Kizuiani, Faraji Omary(26) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kujibu mashtaka manne, likiwemo la kusambaza picha za ngono na kusambaza machapisho yenye ujumbe mchafu unaoharibu maadili ya jamii.
Mshtakiwa huyo amefikishwa mahakamani hapo, jana Desemba 29, 2002 na kusomewa mashtaka yake na wakili wa Serikali Adolf Ulaya, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Rashid Chaungu.
Wakili Ulaya amedai kuwa mshtakiwa anakabiliwa na kesi ya jinai namba 173/2020 na kwamba ameunganishwa na mshtakiwa mwenzake aitwaye Aisha Kiula, ambaye alisomewa mashtaka kama hayo, Desemba 23, 2020.
Akimsomea mashtaka yake, wakili Ulaya amedai kuwa mshtakiwa anadaiwa kutenda makosa yake kati ya Desemba 4 na Desemba 14, 2020 katika eneo la Kariakoo Jiji hapa.
Hata hivyo, mshtakiwa amekana mashtaka yake na kesi yake imeahirishwa hadi Januari 11, 2021 itakapotajwa.
Mshtakiwa amerudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin