WATUMISHI WANNE MAMLAKA YA BANDARI TANZANIA (TPA) MIKONONI MWA TAKUKURU


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuwafikisha mahakamani watu watano wakiwemo wanne watumishi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kwa makosa ya rushwa, uhujumu uchumi na ukwepaji kodi wa Sh.153.5 milioni.


Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu tarehe 31 Agosti 2020 na Doreen Kapwani, Afisa Uhusiano wa Takukuru kwa niaba ya mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo imesema, watumishi hao walikwisha fukuzwa kazi watafikishwa mahakamni leo.

Doreen imetangaza kutafutwa kwa Madaraka Robert Madaraka, aliyekuwa mhasibu wa Bandari ya Kigoma anayetuhumiwa kuhusika katika tuhuma hizo ili aweze kuunganishwa na wenzake.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم