RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KIFO CHA RAIS MSTAAFU WA KENYA ARAP MOI


Rais  Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa niaba ya Watanzania kwa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa pili wa nchi hiyo, Daniel Arap Moi (95).

Moi amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumanne Februari 4, 2020 katika Hospitali ya Nairobi, Kenya alikokuwa anapatiwa matibabu.

Rais Magufuli ametumia akaunti yake ya Twitter kutuma salamu hizo akisema, “kwa niaba ya Serikali na Watanzania nakupa pole Mhe. Rais Uhuru Kenyatta na Wakenya wote kwa kuondokewa na Rais mstaafu Daniel Toroitich arap Moi.”

“Watanzania tutamkumbuka kwa uongozi wake mahiri, jitihada za kuimarisha uhusiano wetu na Kenya na kufufua Jumuiya ya Afrika Mashariki,” ameandika Rais Magufuli


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم