KESI YA VIGOGO CHADEMA YAPIGWA KALENDA


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,  jana ilishindwa kuendelea na ushahidi katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema, akiwemo mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, kutokana na wakili wa washtakiwa hao, Peter Kibatala kutokuwepo mahakamani.

Kibatala alitakiwa jana Ijumaa Agosti 30,2019 kumhoji shahidi wa saba katika kesi hiyo, Victoria Wihenge ambaye ni Ofisa Uchaguzi kutoka Manispaa ya Kinondoni,  lakini hadi kesi hiyo inaahirishwa alikuwa hajatokea Mahakamani.

Uamuzi wa kuahirisha kesi hiyo ulitolewa na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba ambapo aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 10, 11 na 12, 2019 itakapoendelea.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم