TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI


Arsenal wapo tayari kumuuza mshambuliaji wao raia wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, lakini si kwa Manchester United ama Liverpool. (90min.com)
Mshambuliaji wa Ivory Coast Wilfried Zaha, 26, ameiomba klabu yake ya Crystal Palace imruhusu ahamie Arsenal. Palace inamthaminisha streka huyo streka huyo kuwa na thamani ya pauni milioni 80. (Mirror)

Manchester United wanamini kuwa wataweza kukamilisha usajili wa kuwanasa Sean Longstaff, 21, kutoka Newcastle na Bruno Fernandes, 24, kutoka Sporting Lisbon ya Ureno. (Evening Standard)

Real Madrid watalazimika kulipa kitita cha pauni milioni 150 ili kumsajili kiungo Mfaransa Paul Pogba 26, kutoka Manchester United. (Mirror)
Gareth Bale yawezekana akasilia na Real Madrid baada ya klabu hiyo kushindwa kumpata mnunuzi anayemtaka winga huyo mwenye miaka 29. (Mirror)

Chelsea wanampango wa kumtangaza Frank Lampard kuwa kocha wao mpya kabla ya wachezaji kurudi mpaumzikoni wiki ijayo kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao. plan to announce Derby. (Sun)                Lampard ni moja kati ya wachezaji walioichezea Chelsea                                      kwa mafanikio makaubwa

Liverpool wamefikia makubaliano na Sporting ada ya usajili ipatayo pauni milioni 7 ili kumnunua mshambuliaji kinda Rafael Camacho, 19. (Evening Standard)

Kumefanyika mkutano baina ya viongozi wakuu wa Atletico na Real Madrid juu ya usajili wa usajili wa mshambuliaji Antoine Griezmann, 28, kuelekea dimba la Bernabeu. (L'Equipe - in French)Antoine Griezmann kutimkia Barcelona 

Streka wa Colombia Radamel Falcao, 33, anataka kujiunga na timu inayomilikiwa na David Beckham nchini Marekani Miami pale mkataba wake watakapofiki tamati na klabu ya Monaco. (Sun)

Aston Villa wapo tayari kutuma maombi ya kutaka kumsajili beki wa Southampton Matt Targett. (Express and Star)

Kocha wa West Brom Slaven Bilic anamtaka mchezaji mwenzake wa zamani klabuni hapo Julian Dicks kujiunga naye kama sehemu ya benchi la ufundi.. (Express and Star)

CHANZO.BBC SWAHILI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527