BINADAMU ALIYEPONZWA NA 'KULA SANA MISOSI' AKAJIKUTA ANA KILO 980

KEITH Martin raia wa Uingereza ni moja kati ya watu ambao wameweka historia ya kuwa na uzito usio wa kawaida na unene uliopitiliza.

Martini akiwa na miaka 42 alikuwa na kilo zisizopungua 980 na hakuweza kujigeuza alipolala alihudumiwa na watu wa fani tofauti tofauti zaidi ya 7 wakiwemo manesi na watu waliomsaidia usafi.

Akizungumza na jarida la North Sky huko nyumbani kwake Kaskazini mwa Uingereza Martin alieleza kuwa, "Najilaumu mwenyewe, siwezi kumlaumu yeyote ni kosa langu nilikuwa nakula mwenyewe, hakuna aliyeniwekea bunduki kichwani nilifanya mwenyewe" alieleza Martin.

Vyanzo vinaeleza kuwa Martin alifiwa na mama yake akiwa na miaka 16 tu baada ya hapo akaanza kula vyakula vya mafuta na sukari (junk food) kwa lengo la kujifariji hali iliyompelekea kuwa na uzito na unene uliopitiliza.

Hata hivyo Martin alifariki dunia mwaka 2014 akiwa na miaka 44 huku chanzo cha kifo chake kikielezwa kilitokana na tatizo la pumu.

Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527