WAZIRI MKUU ATOA POLE KWA FAMILIA YA MAREHEMU NDEJEMBI


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi Job Lusinde wakati alipowasili nyumbani kwa Mwanasiasa Mkongwe nchini, marehemu Pancras Ndejembi eneo la Kilimani jijini Dodoma kutoa pole kwa familia Desemba 29, 2018. Kushoto ni Mbunge wa Dodoma Mjini na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde na watatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa na Waziri Mstaafu, William Kusila.. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha Mwanasiasa Mkongwe nchini, Pancras Ndejembi, nyumbani kwa marehemu eneo la Kilimani jijini Dodoma, Desemba 29, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole Bibi Leah Pancras Ndejembi, Mjane wa Mwanasiasa Mkongwe nchini, marehemu Pancras Ndejembi wakati alipokwenda nyumbani kwa marehemu eneo la Kilimani jijini Dodoma kutoa pole kwa familia, Desemba 29, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)PMO
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole, Edna Ndejembi ambaye ni binti Mwanasiasa Mkongwe nchini, marehemu Pancras Ndejembi wakati alipokwenda nyumbani kwa marehemu eneo la Kilimani jijini Dodoma kutoa pole kwa familia, Desemba 29, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa na waombolezaji nyumbani kwa Mwanasiasa Mkongwe nchini, marehemu Pancras Ndejembi wakati alipokwenda nyumbani kwa maremu eneo la Kilimani jijini Dodoma kutoa pole kwa familia, Desemba 29, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527