Picha : LHRC YAENDESHA WARSHA KWA WAANDISHI WA HABARI MIKOA MBALIMBALI KUHUSU MASUALA YA HAKI YA KUPATA NA KUTOA TAARIFA

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (Legal and Human Rights Centre - LHRC) kimeendesha warsha kwa waandishi wa habari kutoka mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo waandishi wa habari juu ya sheria mbalimbali zinazoathiri tasnia ya habari nchini Tanzania na kimataifa.

Warsha hiyo ya siku tatu imeanza leo Oktoba 31,2018 na itamalizika Novemba 2,2018 inafanyika katika Ukumbi wa Morogoro Hotel mkoani Morogoro.

Awali akizungumza katika warsha hiyo,Afisa Mradi wa Kuongeza nafasi ya ushiriki wa wananchi Tanzania unaosimamiwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Fortunata Ntwale alisema warsha hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi huo.

Alisema kupitia warsha hiyo ya siku tatu,waandishi wa habari watapata fursa ya kubadilishana uzoefu juu ya sheria na kanuni zinazoratibu haki ya kupata na kutoa taarifa.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI

Afisa Mradi wa Kuongeza nafasi ya ushiriki wa wananchi Tanzania unaosimamiwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Fortunata Ntwale akizungumza wakati wa warsha
kwa waandishi wa habari kutoka mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo waandishi wa habari juu ya sheria mbalimbali zinazoathiri tasnia ya habari nchini Tanzania na kimataifa.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu -LHRC, William Kahale akizungumza wakati wa warsha hiyo.
Afisa Utetezi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu -LHRC, Raymond Kanegene akiandika mwongozo wakati wa warsha hiyo.
Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu -LHRC, William Kahale akitoa mada kuhusu sheria.
Washiriki wa warsha hiyo wakiwa ukumbini.
Warsha inaendelea.
Washiriki wakiwa ukumbini.
Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu -LHRC, William Kahale akiendelea na mada ukumbini.
Kulia ni Mkurugenzi wa Malunde1 blog,Kadama Malunde akizungumza wakati wa warsha hiyo.
Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu -LHRC, William Kahale akitoa mada ukumbini.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527