WATU WAWILI WAUAWA KWA KUPIGWA RISASI KIBITI


Watu wawili wameuawa kwa kupigwa risasi katika kijiji cha Mangwi kilichopo Kata ya Mchukwi wilayani Kibiti mkoani Pwani usiku wa kuamkia leo (Jumatano).

Waliouawa wametajwa kuwa ni Mtendaji wa kijiji hicho, Shamte Makawa na mwenyekiti wa Kitongoji cha Mangwi, Maiko Nicholaus.

Habari za awali zinaeleza maiti ya mwenyekiti huyo wa kitongoji bado haijaonekana na nyumba zao zimechomwa moto.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga amethitisha kutokea kwa mauaji hayo.

Amesema polisi wameenda eneo la tukio kwa ajili ya ufuatiliaji na ukaguzi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments