CHIDI BENZ APELEKWA BAGAMOYO KUSAIDIWA AACHE KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA



Meneja wa Diamond, Babutale akishirikiana na Kalapina wamemchukua Chidi Benz na kumpeleka Life and Hope Rehabilitation Organization iliyopo Bagamoyo kwa ajili kumsaidia kuacha matumizi ya madawa ya kulevya. 




Hatua hiyo imekuja baada ya hivi karibuni rapa huyo kuomba msaada baada ya kuona ameshindwa kukabiliana na matatizo ya kiafya ambayo yamekuwa yakimkabili. 




Kupitia instagram, Babutale amepost video na kuandika:


"Mwana amekubali kukaa Soba ila anasisitiza wana mje kumtembelea kumpa hope na kuleta mapokopoko manjari. Mungu bariki hii safari ya matumaini" 




Katika video hiyo Babu Tale alisema wamefika salama Life and Hope Rehabilitation Organization, Huku Kalapina akiomba mungu kumsaidia Chidi Benz.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527