Christopha Alex Masawe ambaye moja kati ya matukio atakayokumbukwa
na wapenzi wa soka ndani na nje ya nchi ni mkwaju wa mwisho wa penalt
ulioyiondosha katika mashindano ya klabu bingwa barani afrika timu
Zamalek ya Misri ambayo ilikuwa inashikilia ubingwa wa afrika mwaka
2003.
Mwili wa nguli huyo umezikwa katika makaburi ya Nkuhungu na maelfu
ya waombolezaji huku baadhi ya wachezaji waliowahi kucheza nae enzi za
soka lake akiwemo mlinda mlango Juma Kaseja na mlinzi Boniphace Pawasa
pamoja na wadau wa soka nchini wakazungumzia kile walichokifahamu kuhusu
nyota huyu aliyezimika.